#HABARI: Juni 23, 2025, Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameendelea na ziara yake ya kikazi nchini Ujerumani na amekuwa na vikao muhimu sana vinavyolenga kuimarisha ushirikiano kati ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki na UEM, pamoja na kujadili fursa za maendeleo na ushirikiano katika nyanja mbalimbali.

Kwa nyakati tofauti Baba Askofu Dkt. Msafiri Mbilu, amekuwa na vikao na Katibu Mkuu wa UEM, Mch. Dkt. Andar Parlindungan, Naibu Katibu Mkuu UEM anayesimamia Bara la Africa Mch. Dkt. John Wesley Kabango, Mkurugenzi wa Fedha wa UEM, Bwana Timo Pauler pamoja na iliyewahi kuwa meneja wa shamba la Irente farm miaka ya 1991 na kuendelea Bwana Mr. Jeans Pfeil .

UEM: United Evangelical Mission ni chama Cha kiinjili Cha kimisioni kilicho anzishwa mnamo mwaka 1996 na Wamisionari kutoka Ujerumani wa Rhenish na Betheli ambao walifika Africa, na Asia kwa ajili ya kuanzisha shughuli za Dini. Katika Africa walifika katika nchi 7 ambazo ni Tanzania, DR Congo, Africa ya Kusini, Botswana, Cameroon, Namibia na Rwanda kukiwa na madhehebu 15. Katika Tanzania UEM inawakilishwa na Makanisa 4 ya KKKT ambayo ni KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Magharibi, KKKT-Dayosisi ya Mashariki na Pwani pamoja na KKKT-Dayosisi ya Karagwe.

Tufuatilie kwenye mitandao yetu ya kijamii
INSTAGRAM - / elctned
FACEBOOK ACCOUNT North Eastern Diocese
FACEBOOK PAGE - ELCT-North Eastern Diocese
YOUTUBE - / KKKT DKMS Online TV
KWA MAONI NA USHAURI:
Simu : +255 743 399 798

 

Juni 17, 2025 Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ameendelea na ziara yake nchini Ujerumani na amekuwa na Kikao na Mkuu wa Jimbo la Vlotho Mch. Dorothea Goudefroy katika Ofisi ya Jimbo la Vlotho unaitwa Tambarare. Siyo jambo jepesi kupata jina la Mtaa kwenye nchi ya Ujerumani kwani ni lazima vikao vingi vifanyike na mapendekezo yakapitishwe na Wizara inayohusika kwa ngazi zao. Mtaa huu ulizinduliwa Mwaka 2011. Askofu Dkt. Mbilu alishiriki kwenye siku ya Uzinduzi wa Mtaa huu wakati akiwa Mwanafunzi wa PhD nchini Ujerumani.Wakati huo alialikwa kama mwana DKMs kuwa mmoja wa wanaoshirikiana na Meya wa Vlotho pamoja na Mkuu wa Jimbo la Vlotho wa wakati huo Andreas Hunnecke kuzindua Mtaa huu.

 
KATIKA PICHA NI: Ziara ya Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) Dkt. Msafiri Joseph Mbilu,akiwa inchini Ujerumani. Katika ishara ya uhusiano thabiti na wa muda mrefu kati ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki na Kanisa la Westphalia la nchini Ujerumani, Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu alikuwa miongoni mwa viongozi wa Ibada kubwa ya kumsimika Mkuu mpya wa Kanisa la Ujerumani, Bishop Dkt. Adelheid Tuck-Schröder.

Viongozi mbalimbali wa serikali, dini pamoja na wataalam wa Elimu ya watu maalum wenye ulemavu wametakiwa kusimamia na kuhimiza haki na usawa wa kielimu kwa kushirikiana na jamii ili kuondoa dhana potofu katika jamii kuwa watu wenye ulemavu hawana uwezo wa kufanya jambo lolote katika jamii kwasababu ya hali waliyonayo.