Rais wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF) Askofu Henrik Stubkjær ameungana na Watanzania katika kuadhimisha siku ya ugonjwa wa Hemophilia Duniani ambapo jamii imeaswa  kupima mara kwa mara ili kuweza kujua hali ya Afya zao na kuchukua hatua mapema.

 

Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Askofu Dkt. Alex Malasusa amesema kuwa ujio wa Rais wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF), nchini Tanzania Askofu Henrik Stubkjær utaendelea kuimarisha uhusiano uliopo na Makanisa ya Kilutheri  duniani katika kulitangaza neno la Mungu.

Rais wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (Lutheran World Federation “LWF”), Askofu Henrik Stubkjær amewasili nchini Tanzania tayari kuanza ziara yake ya siku 3 ya kuitembelea KKKT,ambapo amepokelewa na  na mwenyeji wake Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania  (KKKT) Askofu Dkt. Alex Gehaz Malasusa .

 
Ufunuo 14:13 “Nikasikia sauti kutoka Mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao”