Uncategorised
- Details
#HABARI: Juni 23, 2025, Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameendelea na ziara yake ya kikazi nchini Ujerumani na amekuwa na vikao muhimu sana vinavyolenga kuimarisha ushirikiano kati ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki na UEM, pamoja na kujadili fursa za maendeleo na ushirikiano katika nyanja mbalimbali.
Kwa nyakati tofauti Baba Askofu Dkt. Msafiri Mbilu, amekuwa na vikao na Katibu Mkuu wa UEM, Mch. Dkt. Andar Parlindungan, Naibu Katibu Mkuu UEM anayesimamia Bara la Africa Mch. Dkt. John Wesley Kabango, Mkurugenzi wa Fedha wa UEM, Bwana Timo Pauler pamoja na iliyewahi kuwa meneja wa shamba la Irente farm miaka ya 1991 na kuendelea Bwana Mr. Jeans Pfeil .
UEM: United Evangelical Mission ni chama Cha kiinjili Cha kimisioni kilicho anzishwa mnamo mwaka 1996 na Wamisionari kutoka Ujerumani wa Rhenish na Betheli ambao walifika Africa, na Asia kwa ajili ya kuanzisha shughuli za Dini. Katika Africa walifika katika nchi 7 ambazo ni Tanzania, DR Congo, Africa ya Kusini, Botswana, Cameroon, Namibia na Rwanda kukiwa na madhehebu 15. Katika Tanzania UEM inawakilishwa na Makanisa 4 ya KKKT ambayo ni KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Magharibi, KKKT-Dayosisi ya Mashariki na Pwani pamoja na KKKT-Dayosisi ya Karagwe.
- Hits: 1298
- Details
Juni 17, 2025 Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ameendelea na ziara yake nchini Ujerumani na amekuwa na Kikao na Mkuu wa Jimbo la Vlotho Mch. Dorothea Goudefroy katika Ofisi ya Jimbo la Vlotho unaitwa Tambarare. Siyo jambo jepesi kupata jina la Mtaa kwenye nchi ya Ujerumani kwani ni lazima vikao vingi vifanyike na mapendekezo yakapitishwe na Wizara inayohusika kwa ngazi zao. Mtaa huu ulizinduliwa Mwaka 2011. Askofu Dkt. Mbilu alishiriki kwenye siku ya Uzinduzi wa Mtaa huu wakati akiwa Mwanafunzi wa PhD nchini Ujerumani.Wakati huo alialikwa kama mwana DKMs kuwa mmoja wa wanaoshirikiana na Meya wa Vlotho pamoja na Mkuu wa Jimbo la Vlotho wa wakati huo Andreas Hunnecke kuzindua Mtaa huu.
- Hits: 1132
- Details

- Hits: 1205
- Details
Viongozi mbalimbali wa serikali, dini pamoja na wataalam wa Elimu ya watu maalum wenye ulemavu wametakiwa kusimamia na kuhimiza haki na usawa wa kielimu kwa kushirikiana na jamii ili kuondoa dhana potofu katika jamii kuwa watu wenye ulemavu hawana uwezo wa kufanya jambo lolote katika jamii kwasababu ya hali waliyonayo.
- Hits: 1300
Page 1 of 117