Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheru Tanzania , Askofu Dkt.Fredrick Shoo. amewasili Wilayani Lushoto Mkoani Tanga ambapo hapo kesho pamoja na maaskofu wengini ataongoza Ibada ya kuwekwa wakfu Askofu Mteule wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu pamoja na kuingizwa kazini kwa msaidizi wa Askofu Mch .Michael Mlondakweli kanju.
Usikose kufuatilia Ibada hii mubashara kupitia Youtube channel yetu ya KKKT DKMs pamoja na Utume fm Radio 97.3 MHz. Matangazo haya ya moja kwa moja yatakujia pia kupitia Radio Sauti ya Injili,Upendo Fm Radio pamoja na Upendo Tv.