"Pandeni milimani, Mkalete miti, mkaijenge nyumba; nami nitaifurahia, nami nitatukuzwa, asema Bwana".Hagai 1:8. Leo tarehe 03/09/2022 Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameongoza harambee ya ujenzi wa Kanisa katika Usharika wa Kabuku, Jimbo la Tambarare. Askofu Dkt. Msafiri Mbilu alianza harambee hiyo kwa kutoa kiasi cha Tsh. 200,000/= (LAKI MBILU). Baada ya harambee yote kufanyika kiasi cha Tshs. 17,695,000/= kilipatikana Ikiwa ni fedha taslimu Tshs. 14,695,000/ huku ahadi ikiwa Tshs. 3,000,000/=