Print

Kuelekea kilele cha uchangiaji wa Tsh 30,000 kwa kila msharika wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki-(KKKT-DKMs) kwa ajili ya kupunguza deni linaloikabili Dayosisi kitakacho fanyika katika Jimbo la Tambarare Usharika wa Korogwe tarehe 17/12/2023. Askofu Dkt Msafiri Mbilu amewashukuru wale wote ambao wameingia kazini kuchangia deni hilo.

Askofu Dkt. Mbilu ameongeza kuwa siku hiyo itakuwa ni kilele cha kukusanya kiasi hicho na kupata taarifa za uchangiaji kwa kila Usharika “Awali ya yote napenda kuwashukuru ninyi wote kwa jinsi mlivyopokea wito huu wa kila mmoja kuchangia Tsh. 30,000/=. Fedha hizi zimesaidia sana kupunguza deni la Dayosisi. Ninapenda kuwajulisha kuwa tutakuwa na siku rasmi ya kilele cha mchango huu wa Tsh. 30,000 tarehe 17/12/2023 kwenye Jimbo la Tambarare Usharika wa Korogwe, wapo watu wengi waliomaliza na kuendelea kuongeza zaidi na zaidi patano la kuchangia kiasi cha Tsh.30,000, lakini pia wapo ambao wameanza lakini hawajakamilisha nawasihi kukamilisha patano letu".Alisema  Askofu Dkt. Mbilu.

Baba Askofu amesisitiza kwa wale wote ambao bado hawajakamilisha mchango wa Tsh. 30,000/= wanaombwa kukamilisha mchango wao kupitia Sharika zao ili siku ya kilele taarifa ya kila Usharika iwasilishwe bila deni, ili kutoa mwanga wa jinsi ya kujipanga na awamu nyingine za uchangiaji.

Kutokana na ukubwa wa deni la Dayosisi harambee hizi zitakuwa endelevu,Baba Askofu anazidi kuwatakia baraka za Mungu ninyi nyote kwa kujitoa kwenu ili kazi ya Mungu iendelee kusonga mbele kwani kwa mshikamano uliopo ipo siku deni hili litakwisha na kurudisha heshima ya Dayosisi yetu.

Hits: 2195