Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu,Tarehe: 11/11/2023, akiwa katika Jimbo la Kusini, Usharika wa Ambangulu, ameongoza Ibada iliyokuwa na tendo la kuwabariki Vijana wa Kipaimara.
Ambapo jumla ya Vijana wapatao 62 wamebarikiwa na wawili kati yao walibatizwa, wakisoma Risala yao kwa Baba Askofu Dkt Msafiri Mbilu, wameeleza kuwa moja ya mafanikio waliyoyapata katika kipindi cha miaka 2 katika darasa lao la Kipaimara ni pamoja na kuandaliwa vema kiimani.
Wameongeza kuwa ili kumshinda mwovu shetani na hila zake wataendelea kusimama katika Imani, kujifunza neno la Mungu kwa kulisoma na kutembea nalo katika maisha yao huku wakiitegemea neema ya Mungu katika kuyatenda mapenzi yake.
 
Katika Ibada hiyo Vijana hao walitoa kiasi cha Tsh 200,000 kwaajili ya kuchangia ulipaji wa deni la Dayosisi, ambapo pia waliomba kuungwa mkono na wazazi,walezi pamoja na washarika walioshiriki katika Ibada hiyo na kufanikiwa kukusanya jumla ya Ths. 1,198,000/= ambapo fedha hizo zimeelekezwa katika kulipa deni la Dayosisi.