
Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu,Tarehe: 12/11/2023, akiwa katika Jimbo la Kusini, Usharika wa Ubiri, ameongoza Ibada iliyokuwa na tendo la kuwabariki Vijana wa Kipaimara.

Ambapo jumla ya Vijana wapatao 29 wamebarikiwa na 3 kati yao wamebatizwa, wakisoma Risala yao mbele ya Baba Askofu Dkt. Msafiri Mbilu vijana hao wamemshukuru Baba Askofu Dkt Msafiri Mbilu kwa kufika na kuungana nao katika siku ya kubarikiwa kwao na wamempongeza Baba Askofu kwa jitihada zake katika kuiongoza na kuiletea maendeleo Dayosisi.

Wameongeza kuwa wana tambua kazi kubwa inayofanywa na KKKT-DKMs katika kumhudumia mwanadamu kiroho, kimwili na kiakili hasa kazi kubwa inayofanyika katika kufufua na kuimarisha vituo vinavyotoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu
.

Katika Ibada hiyo Vijana hao walitoa kiasi cha Tsh 90,000 kwaajili ya kuchangia ulipaji wa deni la Dayosisi, ambapo pia waliomba kuungwa mkono na wazazi,walezi pamoja na washarika walioshiriki katika Ibada hiyo na kufanikiwa kukusanya jumla ya Ths. 1,312,700/= ambapo fedha hizo zimeelekezwa katika kulipa deni la Dayosisi.





