KANISA LA KINJIILI LA KILUTHER TANZANIA
DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI
S.L.P 10,
LUSHOTO.
NAFASI YA KAZI
Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya Kilutheri yaliungana na kuunda Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT). Leo hii KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) ni miongoni mwa Dayosisi 27 ndani ya KKKT. Dayosisi inaitwa hivyo kwakuwa inapatikana Kaskazini Mashariki mwa Tanzania katika Mkoa wa Tanga. Kwahiyo KKKT-DKMs ni taasisi ya kidini iliyosajiliwa tarehe 19 Juni 1963 na Makao yake Makuu yapo Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga. Dhamira ya KKKT-DKMs ni kufundisha na kuhubiri neno la Mungu na kutoa huduma nzuri kiroho, kimwili, kiakili, kiuchumi na kijamii kwa watu. Taasisi hii inatoa tangazo la kazi kwa nafasi ifuatayo:
MTEKNOLOJIA DARAJA LA II-DAWA (NAFASI 1)
MAJUKUMU YA MUOMBAJI
- Kuanisha, kuandaa na kuagiza mahitaji ya dawa na vifaa tiba katika eneo la kazi.
- Kugawa dawa na vifaa tiba kwa wagonjwa na watumishi.
- Kuchanganya dawa.
- Kuhifadhi dawa na vifaa tiba.
- Kuelimisha jamii juu ya matumizi sahihi ya dawa.
- Kukagua dawa, vifaa tiba kemikali, vitendanishi na vipodozi katika eneo lake la kazi.
- Kutoa taarifa juu ya madhara yatokanayo na matumizi ya dawa.
- Kuratibu kazi za kamati ya dawa na vifaa tiba.
- Kuandaa taarifa ya matumizi ya dawa na vifaa tiba.
- Kufanya uchunguzi wa ubora wa dawa, vifaa tiba kemikali, vitendanishi na vipodozi.
- Kufanya kaguzi mbalimbali katika sehemu zinazohifadhi dawa.
- Kusimamia utendaji kazi watumishi walio chini yake.
- Kutunza kumbukumbu za dawa na vifaa tiba.
SIFA ZA MWOMBAJI
- Elimu ya kuanzia Diploma ya ufamasia kutoka chuo kinachotambuliwa na serikali.
- Lazima
- Ajue kutumia software za computer Zaidi kipengele cha Microsoft office.
- Ajue kutumia software zinatumika katika usimamiaji wa dawa.
- Mwenye moyo wa kufanya kazi kwenye mazingira yoyote.
- Umri kuanzia miaka 25 na isiyozidi 40
NAMNA YA KUTUMA MAOMBI.
- Barua ya maombi iambatanishwe na nakala za vyeti vya Elimu, wasifu wa mwombaji (Cv), cheti cha kuzaliwa, na nakala za vyeti vyote vya ujuzi mbalimbali (kama unavyo).
- Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 24/11/2023
- Waombaji watakaokidhi vigezo ndio watakaoitwa kwenye usaili (Interview)
Tarehe ya usaili watajulishwa kwa njia ya simu.
Maombi yote yatumwe kwa Katibu Mkuu-KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki S.L.P 10 LUSHOTO Au: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.