KANISA LA KINJIILI LA KILUTHER TANZANIA

DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI

S.L.P 10,

LUSHOTO.

 

 NAFASI YA KAZI

Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya Kilutheri yaliungana na kuunda Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT). Leo hii KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) ni miongoni mwa Dayosisi 27 ndani ya KKKT. Dayosisi inaitwa hivyo kwakuwa inapatikana Kaskazini Mashariki mwa Tanzania katika Mkoa wa Tanga. Kwahiyo KKKT-DKMs ni taasisi ya kidini iliyosajiliwa tarehe 19 Juni 1963 na Makao yake Makuu yapo Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga. Dhamira ya KKKT-DKMs ni kufundisha na kuhubiri neno la Mungu na kutoa huduma nzuri kiroho, kimwili, kiakili, kiuchumi na kijamii kwa watu. Taasisi hii inatoa tangazo la kazi kwa nafasi ifuatayo:

 

MTEKNOLOJIA DARAJA LA II-DAWA (NAFASI 1)

MAJUKUMU YA MUOMBAJI

  1. Kuanisha, kuandaa na kuagiza mahitaji ya dawa na vifaa tiba katika eneo la kazi.
  2. Kugawa dawa na vifaa tiba kwa wagonjwa na watumishi.
  3. Kuchanganya dawa.
  4. Kuhifadhi dawa na vifaa tiba.
  5. Kuelimisha jamii juu ya matumizi sahihi ya dawa.
  6. Kukagua dawa, vifaa tiba kemikali, vitendanishi na vipodozi katika eneo lake la kazi.
  7. Kutoa taarifa juu ya madhara yatokanayo na matumizi ya dawa.
  8. Kuratibu kazi za kamati ya dawa na vifaa tiba.
  9. Kuandaa taarifa ya matumizi ya dawa na vifaa tiba.
  10. Kufanya uchunguzi wa ubora wa dawa, vifaa tiba kemikali, vitendanishi na vipodozi.
  11. Kufanya kaguzi mbalimbali katika sehemu zinazohifadhi dawa.
  12. Kusimamia utendaji kazi watumishi walio chini yake.
  13. Kutunza kumbukumbu za dawa na vifaa tiba.

 SIFA ZA MWOMBAJI

  • Elimu ya kuanzia Diploma ya ufamasia kutoka chuo kinachotambuliwa na serikali.
  • Lazima
  • Ajue kutumia software za computer Zaidi kipengele cha Microsoft office.
  • Ajue kutumia software zinatumika katika usimamiaji wa dawa.
  • Mwenye moyo wa kufanya kazi kwenye mazingira yoyote.
  • Umri kuanzia miaka 25 na isiyozidi 40

 NAMNA YA KUTUMA MAOMBI.

  1. Barua ya maombi iambatanishwe na nakala za vyeti vya Elimu, wasifu wa mwombaji (Cv), cheti cha kuzaliwa, na nakala za vyeti vyote vya ujuzi mbalimbali (kama unavyo).
  2. Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 24/11/2023
  3. Waombaji watakaokidhi vigezo ndio watakaoitwa kwenye usaili (Interview)

Tarehe ya usaili watajulishwa kwa njia ya simu.

 Maombi yote yatumwe kwa  Katibu Mkuu-KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki S.L.P 10 LUSHOTO Au: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.