Print

Mei 9 mwaka 2021 ilikuwa ni siku iliyotawaliwa na nderemo, vifijo na shamrashamra katika viunga vya Lushoto, siri nyuma ya furaha hii si nyingine bali ni historia mpya kuandikwa, wakristo wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki walipata Askofu mpya, kiongozi ambae atayabeba maono na dira ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki huyu sio mwingine bali ni Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu.

Baba Askofu Dkt. Mbilu, aliingizwa kazini katika Ibada iliyofanyika Kanisa Kuu Lushoto tarehe 09/05/2021, na kisha yeye kumuingiza kazini msaidizi wake, Mch. Michael Mlondakweli Kanju. sasa leo tarehe 09/05/2024 ni miaka mitatu ya Uongozi wa Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu tangu alipopewa kibali na Mungu cha kuiongoza KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.
 
Leo tarehe 09/05/2024 zimetimia siku 1,096, yaani miaka mitatu tangu alipoingizwa kazini kushika wadhifa huo , bado tunaiona shauku ileile ndani yake kwani licha ya kusimamia mafundisho sahihi ya Neno la , Askofu Dkt. Mbilu amesimamia msingi wa Dayosisi katika kumhudumia mwanadamu kimwili, kiakili na kiroho.

Askofu Dkt. Mbilu licha ya kusimamia Dayosisi kupitia kauli mbiu yake ya kasi tofauti, ameendelea kuwa mnyenyekevu na msikivu kwa washarika wote  kwani anaamini ushirikiano mzuri wanaompa ndio msingi wa mafaniko ya Dayosisi.

 
Hits: 9477