
Askofu Dkt. Mbilu ametoa wito huo tarehe 28-9-2024 wakati akitoa salamu kwa waumini wa KKKT-DKMs katika Ibada ya Kustaafu kwa heshima Mchungaji Ezekiel Andrea Mwarabu iliyofanyika katika Usharika wa Hale Jimbo la Tambarare na kukazia kuwa hakuna mtu mwenye haki ya kutenda ukatili kwa mwingine ikiwemo mauwaji.
Amesema kwa msaada wa Mungu na maombi Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itafanikiwa kuwabaini na kuwakamata wale wote waliohusika katika matukio hayo yanayo ichafua nchi.
Katika hatua nyingine amewakumbusha watumishi wa KKKT-DKMs kuendelea kutumika kwa uaminifu na kutenda haki katika wajibu wao kama walivyoapa wakati wa kuingizwa kazini jambo litakalowaongoza kuwa na mwisho mwema na kustaafu kwa heshima kama ilivyokuwa kwa Mch.Mstaafu Ezekiel Mwarabu aliyelitumikia Kanisa kwa miaka 29 .
Amesema pamoja na kutumika madhabauni lakini pia watumishi katika Kanisa wanapaswa kujishughulisha na shughuli nyingine halali za kiuchumi zitakazo saidia boresha hali zao za maisha bila kuharibu wito mkuu wa kumtumikia Mungu.
Ibada hii ya Kustaafu kwa Mchungaji Ezekiel Andrea Mwarabu pia ilihudhuriwa na Msaidizi wa Askofu Mch. Michael Mlondakweli Kanju, Katibu Mkuu wa KKKT-DKMs Mwl. Julius Madiga, Wakuu wa Majimbo, Wachungaji, Wainjilisti, Mashemasi na Washarika wawakilishi kutoka Majimbo yanayounda KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.
