![]()
Kikao cha Halmashauri ya Kurugenzi ya Huduma za Jamii – KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kimefanyika tarehe 05 Desemba 2025 katika ukumbi mdogo wa mikutano wa Utondolo, Lushoto.
Kikao hiki kimeonesha kwa namna ya pekee jinsi Kurugenzi hii inavyotekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kusimamia kwa weledi vituo mbalimbali vya huduma ambavyo vimeendelea kuleta manufaa makubwa kwa Kanisa na kwa jamii ya Watanzania kwa ujumla.
Katika kikao hicho, wajumbe walijadili kwa kina mikakati ya kuboresha na kukuza huduma katika vituo vyote vilivyo chini ya Dayosisi. Mkurugenzi wa Huduma za Jamii, Mwl. Afizai Vuliva, aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Kurugenzi kwa lengo la kupokea ushauri na maoni ya wajumbe. Taarifa hiyo imeonesha hatua kubwa zilizopigwa, changamoto zilizopo, pamoja na maeneo yanayohitaji kuimarishwa ili kuongeza tija na ubora wa huduma kwa Kanisa na jamii kwa ujumla. Kurugenzi ya Huduma za Jamii inasimamia na kuratibu idara muhimu zinazogusa maisha ya Kanisa na Jamii moja kwa moja, zikiwemo:
- Idara ya Elimu
- Idara ya Afya
- Idara ya Jinsia na Watoto
- Diakonia (Huduma za Uangalizi na Uchangiaji kwa Jamii)
- Idara ya Vijana na UKWATA
Kupitia usimamizi makini wa Kurugenzi hii, vituo hivi vya huduma vya Dayosisi vimeendelea kuimarika na kutoa huduma zenye kiwango bora, hivyo kuifanya KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kuwa mfano wa kuigwa katika utoaji na usimamizi wa huduma za kijamii.
Tufuatilie kwenye mitandao yetu ya kijamii
INSTAGRAM - / elctned
FACEBOOK ACCOUNT North Eastern Diocese
FACEBOOK PAGE - ELCT-North Eastern Diocese
YOUTUBE - / KKKT DKMS Online TV
WEBSITE: www.elctned.org
KWA MAONI NA USHAURI:
Simu : +255 743 399 798