
MATUKIO KATIKA PICHA TAREHE 02/11/2023:- Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu pamoja na kikundi cha Wadiakonia 30 kutoka Ujerumani ambao wameitembela Dayosisi yetu na wamepata nafasi ya kutembelea shule ya Msingi ya Irente Rainbow School inayomilikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.Baba Askofu amewashukuru wadiakonia hawa wenyeurafiki na shule hii kwa namna wanavyojitoa kwa hali na mali katika kuchangia maendeleo ya shule hiyo.Katika kuchangia maendeleo na kazi mbalimbali katika shule hiyo wadiakonia hawa wametoa kiasi cha Tsh: 7,891,200.







