Print

 

TANGAZO LA ZABUNI YA UNUNUZI WA MADINI YA DHAHABU – BANGALA

Katibu Mkuu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, anapenda kuwatangazia wazabuni na makampuni yenye sifa ndani na nje ya Wilaya ya Lushoto kwamba yanakaribishwa kutuma maombi ya zabuni ya kununua madini aina ya Dhahabu katika kata ya Vuga Kijiji cha Kihitu- Bangala (Eneo linalo milikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki).Mwombaji aambatanishe kivuli cha leseni hai ya biashara na hati ya usajili ya mlipa kodi (TIN) na aoneshe eneo lake la biashara (Physical Address).Utaratibu wa kutuma maombi, tuma maombi katika bahasha na isioneshe alama yoyote ya utambulisho wa mwombaji. Ada ya maombi ni Tsh. 30,000 itumwe kwenye akaunti namba 41606600224 NED-ELCT MFUKO WA FAIDA.Tuma maombi yako kwa,Katibu Mkuu KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,S.L.P 10 Lushoto,Maombi yatumwe kabla ya tarehe 25/03/2022