Print
KATIKA PICHA: Ibada ya Jumapili ya tarehe 10/03/2024 kutoka Usharika wa St. Marien Minden nchini Ujerumani, ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu nchini humo.
Pamoja na mambo mengine yaliyojadiliwa katika Usharika huo Baba Askofu pamoja na mwenyeji wake wamekamilisha maandalizi ya ziara ya Vijana 11 kutoka katika Dayosisi yetu watakaotembelea nchi ya Ujerumani kuanzia tarehe 14. Aprili hadi tarehe 6. Mei 2024.
Vijana hao11 kutoka KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Usharika wa Mtae watakuwa na Kongamano la maswala ya Maji nchini Ujerumani. Kongamano hili litasimamiwa na Usharika wa St. Marien Minden.