Print

Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.

Ufunuo 14:13

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, leo tarehe 16/04/2022 akiwa katika Usharika wa Mlalo Jimbo la Kaskazini ameongoza Ibada ya mazishi ya Balozi Fanuel Ismail Kuzilwa.

 

Balozi Fanuel  Kuzilwa aliyezaliwa tarehe 21/07/1945 ameitwa mbinguni tarehe 12/04/2022, akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

KATIKA UTUMISHI: Marehemu Balozi Kuzilwa  katika uhai wake aliwahi kushika nafasi mbalimbali za kiuongozi, aliwahi kuwa Afisa Mwandamizi- Ubalozi wa Tanzania Nchini Angola na Nigeria.KATIKA TEUZI ZA RAIS aliteuliwa kuwa – Mkurugenzi wa Idara ya Africa, Wizara ya Mambo ya nje,Mnikulu, Balozi.Hata hivyo uongozi wa KKKT-DKMs utaendelea kumkumbuka Marehemu Balozi Kuzilwa kwa juhudi zake katika kuhakikisha Chuo Kikuu cha SEKOMU kinafunguliwa.

Uongozi wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, unatoa pole kwa Familia ya Marehemu Balozi Fanuel Kuzilwa, ndugu jamaa na marafiki wote walioguswa na msiba huu mzito. Mungu awape nguvu na faraja ya kweli katika kipindi hiki kigumu. BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe.