ELCT North Eastern Diocese
Ibada ya Kipaimara Usharika wa Kana, Youths Confirmation at Kana Lutheran Parish
- Details
“……Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.”
Leo tarehe 07/11/2021 imekuwa siku ya baraka kwa washarika wa Usharika wa Kana, Jimbo la Pwani, ambapo vijana wapatao 33 walibarikiwa na mmoja kati yao alibatizwa.
- Hits: 10192
TANZIA-
- Details
"Naye atafuta kila chozi katika macho yao,wala mauti haitakuwepo tena,wala kilio, wala maumivu hayatakuwepo tena, kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita " UFUNUO 21:4.
Kaimu Katibu Mkuu wa KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Godfrey Tahona Walalaze kwa niaba ya Uongozi wa KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki anasikitika kutangaza kifo cha Mama Mzazi wa Mch.Juliana Mahundo, Bi. Raheli Mahundo, kilichotokea tarehe 05/11/2021.
Ibada ya mzishi itafanyika siku ya Jumatatu tarehe 08/11/2021katika mtaa wa Mindu, Usharika wa Kwabada-Muheza.
Uongozi unatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki popote pale walipo. BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe.
- Hits: 7846
Pumzika kwa amani Mzee Tamilwai Agustino Baruti
- Details
TANZIA
"Naye atafuta kila chozi katika macho yao,wala mauti haitakuwepo tena,wala kilio, wala maumivu hayatakuwepo tena, kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita " UFUNUO 21:4.
Kaimu Katibu Mkuu wa KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Godfrey Tahona Walalaze kwa niaba ya Uongozi wa KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki anasikitika kutangaza kifo cha Baba Mzazi wa Mch. Lemmy Baruti, Mzee Tamilwai Augustino Baruti kilichotokea usiku wa tarehe 31/10/2021 katika hospitali ya Wilaya ya Pangani.
Taratibu za mazishi zinaendelea na mtajulishwa.
Uongozi unatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki popote pale walipo. BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe.
........... ................ ................. .....................
- Hits: 8393
Ibada ya Kipaimara KKKT-DKMs,Usharika wa Irente
- Details
Leo tarehe 31/10/2021 imekuwa siku ya baraka kwa washarika wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Usharika wa Irente Jimbo la Kusini ambapo vijana wapatao 24 walipata kipaimara.
- Hits: 8800
Page 70 of 107