ELCT North Eastern Diocese
PICHA RASMI YA ASKOFU: Dkt. Msafiri Joseph Mbilu
- Details
Picha rasmi ya Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ,wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, nakala halisi iliyochapishwa Inapatika Makao Makuu ya KKKT-DKMs. Kwa mawasiliana wasiliana nasi kupitia This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. au 0764105944/0655449481
Picha hii ndio itatumika katika Ofisi zote za Sharika za KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki
- Hits: 8608
Ibada ya Kipaimara Usharika wa Kisosora,Youths Confirmation at Kisosora Lutheran Parish.
- Details
Leo tarehe 12/09/2021 imekuwa siku ya baraka kwa washarika wa Usharika wa Kisosora Jimbo la Pwani. Ambapo imefanyika Ibada iliyokuwa na matukio mbalimbali vijana wapatao 19 wamepata kipaimara na wawili kati yao walibatizwa.
- Hits: 9408
Nafasi za masomo Seminari ndogo ya Bangala
- Details
Uongozi wa Shule ya Seminari ndogo ya Bangala iliyopo Halmashauri ya Bumbuli Vuga inawatangazia nafasi za kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka wa masomo 2022 kwa vijana waliomaliza darasa la saba mwaka huu 2021, mtihani wa kujiunga utafanyika tarehe 11/09/2021 na tarehe 25/09/2021. fomu za kujiunga zinapatikana katika vituo vifuatavyo.
Shuleni Bangala,Tumaini Bookshoop(Lushoto),Korogwe , Muheza, Handeni, Makorora, Kana.Pia tuna nafasi chache za wanaopenda kuhamia katika shule yetu kwa kidato cha tatu.
- Hits: 9736
Ziara ya kikazi Shule ya Sekondari Lwandai
- Details
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Dkt. Msafiri Joseph Mbilu leo tarehe 30/08/2021 amefanya ziara ya kikazi katika Shule ya Sekondari Lwandai. Katika ziara hiyo Baba Askofu Mbilu alitembelea mazingira ya Shule na kupokea taarifa iliyowasilishwa na Mkuu wa Shule hiyo, Mch. Daniel Mwarabu na waandamizi wa idara mbalimbali za shule hiyo.
- Hits: 8053
Page 75 of 107