ELCT North Eastern Diocese
Toggle Navigation
  • Home
  • Our Diocese
  • Wopa
  • Gallery
  • Institutions
    • Irente Children's Home
    • Irente School for the Blind
    • Rainbow School
    • Lwandai Secondary School
    • Lutindi Mental Hospital
    • Bangala Lutheran Junior Seminary
    • Bumbuli Hospital
    • SEKOMU university
    • Namna ya kuchangia kazi za maendeleo na Vituo vya kutoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu (KKKT-DKMs)
  • Calendar
  • Projects
    • Irente Biodiversity Reserve
    • UTC - Usambara Technological Center
    • Restaurants and Hostels
      • Tumaini Mbuyukenda Hostel and Restaurant
      • Martin Luther Garden and Restaurant
      • Tumaini Songe Restaurant and Hostel
      • Hohen Restaurant and Hostel
      • Tumaini Lushoto Restaurant and Hostel
  • Superintendent
    • Coast Superintendent
    • Northern Superintendent
    • Southern Superintendent
    • Plains Superintendent
  • New-clips
  • Contact us
  • You are here:  
  • Home

Bishop Rev.Dr. Msafiri J. Mbilu

Change Language

English German Spanish Swahili Swedish

News & Updates

  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI YA KAZI Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya...
  • Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji  NSSF

    Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji NSSF

    Leo tarehe 01/04/2026, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amepokea ugeni kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifa...
  • TAARIFA

    TAARIFA

    Uongozi wa KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ukiwakilishwa na Katibu Mkuu Mwl. Julius Madiga, u...
  • ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Dkt. Msafiri Jos...
  • Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Dayosisi yetu imepata heshima kubwa ya kushiriki katika Mkutano wa Kanda ya Afrika ulioandaliwa na U...

.



 

 

Staff Email

ELCT North Eastern Diocese

Uanzishwaji wa kozi ya muziki KOTETI maandalizi yanaendelea vizuri

  • Print
Details
Published: 22 January 2025

HABARI KWA UFUPI: Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu,amesema kuwa mipango ya uanzishwaji wa kozi ya muziki katika Taasisi ya Elimu ya Kolowa Technical Training Institute (KOTETI) inaendelea vizuri ikiwa ni pamoja na vifaa vitakavyo tumika katika kufundishia kuanza kupatikana.

Askofu Dkt. Mbilu ameyasema hayo leo tarehe 22/01/2025 akiwa katika Ofisi za Makao Makuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki yaliyopo Wilayani Lushoto Mkoa wa Tanga, mara baada ya kupokea ugeni wa marafiki kutoka Bethel Ujerumani.

Ugeni huu unaongozwa na Bw.Werner Jakob Blauth, ambaye alishaawahi kufanya kazi katika kituo cha Lutindi Mental Hospital kinachomilikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.

Aidha Askofu Dkt. Mbilu, ameongeza kuwa ugeni huo umetembelea KKKT-Dayosisi Kaskazini Mashariki kwa lengo la kuona baadhi ya vituo vya Diakonia vya Dayosisi ikiwemo kituo cha Irente children's Home, Irente Rainbow School, Irente School for the Blind pamoja na Hospital ya wagonjwa wa akili (Lutindi Mental Hospital) ili kujionea shughuli mbalimbali zinazofanyika katika vituo hivyo.

Vifaa vilivyo pokelewa leo ni pamoja na Tarumbeta filimbi vikiwa ni alama tu ya vifaa vingine vingi vya muziki ambavyo vipo nchini Ujerumani vikiwa katika hatua za mwisho kusafirishwa kuja katika Dayosisi yetu.

Hata hivyo Askofu Dkt. Msafiri Mbilu, amewashukuru wageni hao kwa mchango wao mkubwa wa kutoa vifaa hivyo vya muziki ikiwa ni ishara ya kuendelea kuonyesha ushirikiano mzuri uliopo kati ya Dayosisi na marafiki hao kutoka Ujerumani.

Hits: 7118

Kuelekea Ibada ya kuwekwa wakfu Askofu wa KKKT-Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria (Mwanza)

  • Print
Details
Published: 18 January 2025
KATIKA PICHA: Ibada illiyokuwa na tendo la kuweka wakfu vifaa vya kiaskofu iliyofanyika KKKT-Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria (Mwanza) Usharika wa Imani Kanisa Kuu. Ibada hii iliongozwa na Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu.
Hits: 8294

Read more ...

Picha ya pamoja mara baada ya Mkutano wa Halmashauri ya Utumishi ya KKKT

  • Print
Details
Published: 16 January 2025

Walioketi ni Katibu Mkuu wa KKKT, Bw. Rogathe Mollel, Askofu wa KKKT-DKMS ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Halmashauri hii ya Utumishi ya KKKT Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, pamoja Katibu Mkuu Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Shinyanga Bi. Happiness Geffi  ambaye ndiye Katibu Mwandishi wa Halmashauri ya Utumishi KKKT. Mkutano huu umefanyika tarehe 16/01/2025 katika Ukumbi wa New Safari Hotel Arusha. 

Hits: 7517

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi aitembelea KKKT-DKMs

  • Print
Details
Published: 02 January 2025

 

Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu,akisalimiana na  Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe.mara baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi za Mkao Makuu ya KKKT-DKMs Lushoto Tanga.

Hits: 7432

Read more ...

  1. HERI YA MWAKA MPYA 2024
  2. Mashindano ya Baiskeli Jimbo la Tambarare 21 DEC 2024
  3. Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Halmashauri Kuu ya KKKT-DKMs watembelea kituo cha Irente Children's Home pamoja na Irente School for the Blind
  4. Askofu Dkt. Mbilu apigakura kuchagua viongozi kwenye uchaguzi wa serikali za mtaa

Page 14 of 137

  • 9
  • ...
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • ...
  • 16
  • 17
  • 18

Back to Top

© 2026 ELCT North Eastern Diocese