KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA

DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI

S.L.P 10, (SIMU 027-266002 / Fax 027-2660092), LUSHOTO.

This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

TANGAZO LA KAZI NAFASI YA BWANA SHAMBA KITUO CHA IRENTE FARM

Irente Farm ni kituo cha kilimo kinachomilikiwa na kuendeshwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT–DKMs), kilichopo Lushoto, Mkoani Tanga. Kituo hiki ni sehemu ya huduma za maendeleo ya jamii zinazotekelezwa na Dayosisi kupitia miradi ya kilimo endelevu. Katika kuimarisha ufanisi wake, kituo kinatangaza nafasi ya kazi kwa cheo cha Bwana Shamba. Tunakaribisha maombi kutoka kwa watu wenye sifa, uwezo, na maadili mema ya Kikristo kushiriki katika huduma hii muhimu.

Majukumu ya Msingi:

  • Kusimamia shughuli zote za kilimo katika shamba la Irente.
  • Kupanga, kuratibu na kufuatilia shughuli za uzalishaji wa mazao na ufugaji.
  • Kusimamia matumizi bora ya rasilimali za shamba (wafanyakazi, vifaa, mbegu, mbolea n.k).
  • Kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu mbinu bora za kilimo na ufugaji.
  • Kuandaa ripoti za maendeleo ya kilimo kwa uongozi wa Irente Farm.
  • Kushirikiana na taasisi na wadau mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya kilimo.

Sifa za Mwombaji:

  • Awe na shahada (degree) katika Kilimo au fani zinazohusiana, kutoka Chuo kinachotambulika na Serikali.
  • Awe na uzoefu wa angalau miaka miwili (2) katika kusimamia shughuli za kilimo na ufugaji.
  • Awe na uwezo wa kutumia kompyuta na kuandaa ripoti za kazi.
  • Awe tayari kuishi na kufanya kazi Irente – Lushoto.

 Namna ya Kutuma Maombi:

Maombi yote yaambatane na:

  • Barua ya maombi
  • Wasifu binafsi (CV)
  • Nakala ya vyeti vya kitaaluma
  • Nakala ya cheti cha kuzaliwa au NIDA

Maombi yote yatumwe   kwa:


Katibu Mkuu,
KKKT– Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,
S.L.P 10,
LUSHOTO – TANGA

Barua pepe: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Mwisho wa Kutuma Maombi: Tarehe 15 Agosti 2025 (saa 9:59 alasiri)

Kumbuka:

Ni waombaji waliokidhi vigezo watakaoitwa kwenye usaili. Kanisa linahimiza usawa wa kijinsia – Wanawake pia wanahamasishwa kuomba nafasi hii.