Kupitia kikao cha Halmashauri Kuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, kilicho fanyika katika ukumbi wa mikutano Utondolo-Lushoto mnamo tarehe 09-10/12/2021 wajumbe wa Halmashauri walipatana kwa kauli moja na kuridhia mwaka 2022 uwe mwaka wa wanawake katika Dayosisi kwa kutambua kuwa Wanawake ni Jeshi kubwa na lililo imara hivyo wanao uwezo wa kuweka mipango mbalimbali endelevu ili kuinua na kuijenga Dayosisi yetu.

Kwa nyakati tofauti Askofu wa KKKT-DKMs Mch. Dkt, Msafiri Joseph Mbilu ametoa akitoa wito kwa Wanawake wote kuupokea kuanzia kwenye ngazi za Mitaa, Sharika, Majimbo hadi Dayosisi kwa kuamini kuwa Wanawake wataweka mipango mbalimbali ili kuuenzi.
 
Usharika wa Mikanjuni uliopo katika Jimbo la Pwani, kupitia Mchungaji wa Usharika huo Mch Jeremiah Mboko wamefanya uzinduzi wa mwaka wa Wanawake leo tarehe 30/01/2022 katika Ibada ya Jumapili.Uzinduzi huo ulifanyika kwa njia ya maombi pamoja na sadaka ya kumshukuru Mungu kama alama ya itikio la Wanawake wa Usharika huo kuupokea mwaka wao.

Katika Ibada hiyo jumla ya Wanawake 346 walishiriki Mch. Mboko aliwasisitiza Wanawake wa Usharika huo kutumia vipawa walivyojaliwa na Mungu  katika Kanisa na jamii kwa ujumla,amesema kuwa anatarajia kuwaona wanawake wakishirikiana kwa wingi katika mikusanyiko na katika kazi mbalimbali za Usharika,Jimbo na Dayosisi kwa ujumla.

.

Idara ya Vijana KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Jimbo la Pwani imefanya mkutano mkuu wa vijana ulikuwa na agenda ya uchaguzi wa viongozi wa vijana ngazi ya jimbo leo tarehe 27 Machi,2021 katika Usharika wa Kana Tanga.

Walio chaguliwa ni Bi.Monica Kitururu mwenyekiti kutoka Usharika wa Kana, Godchance Makamu  kutoka Usharika wa Makorora  .Jausia Mziray  Katibu kutoka Mission ya mto Pangani,Msuya ,Katibu Msaidizi kutoka Usharika wa Pangani na Anzamen Kileo  kutoka Usharika wa Kana amechaguliwa kuwa Mtunza hazina.

 WAJUMBE NI.

  1. Roda Yohana- Bethlehem
  2. Isaya Kifua Maramba

Viongozi mbali mbali wa vijana kutoka sharika za Jimbo la Pwani

Mwenyekiti wa vijana ngazi ya jimbo Bi.Monica Kitururu, akiwashukuru wajumbe mara baada ya uchaguzi.

 

 

 

Mkuu wa jimbo la Pwani (KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ) Mch. Thadeus Ketto  akisaini kitabu cha maombolezo na kutoa heshima za mwisho kwa HAYATI RAIS DR. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga .