ELCT North Eastern Diocese
Toggle Navigation
  • Home
  • Our Diocese
  • Wopa
  • Gallery
  • Institutions
    • Irente Children's Home
    • Irente School for the Blind
    • Rainbow School
    • Lwandai Secondary School
    • Lutindi Mental Hospital
    • Bangala Lutheran Junior Seminary
    • Bumbuli Hospital
    • SEKOMU university
    • Tanga Technical Institute
  • Calendar
  • Projects
    • Irente Biodiversity Reserve
    • UTC - Usambara Technological Center
    • Restaurants and Hostels
      • Tumaini Mbuyukenda Hostel and Restaurant
      • Martin Luther Garden and Restaurant
      • Tumaini Songe Restaurant and Hostel
      • Hohen Restaurant and Hostel
      • Tumaini Lushoto Restaurant and Hostel
  • Superintendent
    • Coast Superintendent
    • Northern Superintendent
    • Southern Superintendent
    • Plains Superintendent
  • New-clips
  • Contact us
  • WELCOME KOTETI
    +255 747 067 564
  • You are here:  
  • Home

Bishop Rev.Dr. Msafiri J. Mbilu

Change Language

English German Spanish Swahili Swedish

News & Updates

  • Nafasi za masomo kwa muhula mpya 2023-2024 Chuo cha Kolowa Technical Training Institute (KOTETI)

    Nafasi za masomo kwa muhula mpya 2023-2024 Chuo cha Kolowa Technical Training Institute (KOTETI)

  • Askofu Dkt. Mbilu, awaasa wazazi na walezi  kuwapeleka watoto wao shule

    Askofu Dkt. Mbilu, awaasa wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao shule

    Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amewasihi wazazi na wal...
  • TAARIFA KWA UMMA

    TAARIFA KWA UMMA

    TAARIFA KWA UMMA Ofisi ya Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbi...
  • Tangazo la nafasi za kazi KKKT-DKMs

    Tangazo la nafasi za kazi KKKT-DKMs

    KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA-DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI [KKKT-DKMs]z UTANGULIZI Tar...
  • Tangazo la nafasi ya kazi DAKTARI DARAJA LA II

    Tangazo la nafasi ya kazi DAKTARI DARAJA LA II

    TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI.. UTANGULIZI Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa me...

Lwandai Sec School

Online TV

 

KOTETI

 

Album pictures

Utume Fm Radio

 



 

 

Staff Email

ELCT North Eastern Diocese

Nafasi za masomo kwa muhula mpya 2023-2024 Chuo cha Kolowa Technical Training Institute (KOTETI)

  • Print
Details
Published: 31 January 2023

Hits: 157

Askofu Dkt. Mbilu, awaasa wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao shule

  • Print
Details
Published: 30 January 2023

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amewasihi wazazi na walezi wenye watoto waliofaulu kwenda kidato cha kwanza kuhakikisha watoto wanakwenda shule ili kupata haki yao ya kupata elimu.

Ameyasema hayo katika Ibada ya Jumapili ya tarehe 29/01/2023 iliyofanyika katika Jimbo la Kusini Usharika wa Mamba na kuwakumbusha waumini kuwa ni jukumu na wajibu wa kila mzazi au mlezi kumpatia mtoto wake elimu.

Hata hivyo Askofu Dkt. Mbilu amewataka pia waumini wote wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki na jamii kwa ujumla kuhakikisha kila mmoja anajiunga na bima ya Afya kwa wote pindi Serikali itakapo kamilisha mchakato huo wenye lengo la kutaka kuhakikisha wananchi wote wanakuwa na bima.

Hits: 200

TAARIFA KWA UMMA

  • Print
Details
Published: 28 January 2023

TAARIFA KWA UMMA

Ofisi ya Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu inawaomba kupuuza ujumbe wa uzushi unaotumwa kwenye simu ukihusisha maneno yafuatayo.

Bwana yesu asifiwe mtumishi,upo wapi muda huu?.naomba unijibu kwa sms nipo kikaoni.ASK.DKT.MSAFIRI MBILU.

Mtu huyo mwenye namba 0693289600 anatumia jina la Askofu Dkt. Msafiri Mbilu kuomba hela na punde anapo jibiwa huandika.

Amen, naomba nikupe namba ya mtu unisaidie kumtumia elfu 40.nikitoka kikaoni nitakupa.

Askofu Dkt. Mbilu hajatuma ujumbe huo pamoja na kusikitishwa  na kitendo hiki  hivyo basi mnataarifiwa kupuuza ujumbe huo.

 

Hits: 315

Tangazo la nafasi za kazi KKKT-DKMs

  • Print
Details
Published: 26 January 2023

KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA-DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI [KKKT-DKMs]z

  1. UTANGULIZI

Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya Kilutheri yaliungana na kuunda Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT). Leo hii KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) ni miongoni mwa Dayosisi 27 ndani ya KKKT. Dayosisi inaitwa hivyo kwakuwa inapatikana Kaskazini Mashariki mwa Tanzania katika Mkoa wa Tanga. Kwahiyo KKKT-DKMs ni taasisi ya kidini iliyosajiliwa tarehe 19 Juni 1963 na Makao yake Makuu yapo Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga. Dhamira ya KKKT-DKMs ni kufundisha na kuhubiri neno la Mungu na kutoa huduma nzuri kiroho, kimwili, kiakili, kiuchumi na kijamii kwa watu. Taasisi hii inatoa tangazo la kazi kwa nafasi zifuatazo:

  1. AFISA MIPANGO WA DAYOSISI

MASHARTI YA JUMLA YA WAOMBAJI WA KAZI.

  1. Awe raia wa Tanzania.
  2. Awe na umri usiopunguza miaka 18 na usiozidi miaka 45.
  • Awe na vyeti kamili vya mafunzo ya fani aliyosomea (Cheti cha Kidato Cha Nne, Sita na Taaluma aliyosomea.
  1. Elimu kiwango cha kuanzia astashahada moja ya uchumi na fani zinazoendana na hizo kutoka vyuo vinavotambulika
  2. Awe na uzoefu usiopungua miaka mitatu
  3. Awe na uzoefu wa kubuni na kuandika miradi pamoja na usimamizi pmoja na tathmini.

MAOMBI YOTE YAAMBATANISHWE NA,

  1. Nakala ya cheti cha kuzaliwa.
  2. Nakala ya cheti cha kidato cha nne au/ na cha sita au stashahada kulingana na kada ya mwombaji. Kwa aliyesoma nje ya nchi au mitaala ya nje ya nchi waambatanishe cheti cha ithibati kutoka baraza la mitihani Tanzania (NECTA).
  • Nakala ya vyeti vya Taaluma na Transcript, Aidha waliosoma vyuo vya nje ya nchi, waambatishe cheti cha Ithibati kutoka TCU.
  1. Wasifu (CV).
  2. Picha ndogo (passport size) moja ya hivi karibuni.
  3. Nakala ya kitambulisho cha uraia (NIDA/ Namba ya NIDA).
  • Iwapo majina yako yanatofautiana katika vyeti vyako Pamoja na cheti cha kuzaliwa na NIDA hakikisha unawasilisha kiapo cha majina (Deed Pool) kutoka kwa Msajili wa viapo na kusajiliwa na Msajili wa hati, wizara ya Ardhi na maendeleo ya makazi.

 

  1. MRATIBU WA MADINI KKKT-DKMs

MASHARTI YA JUMLA YA WAOMBAJI WA KAZI.

  1. Awe raia wa Tanzania.
  2. Awe na umri usiopunguza miaka 18 na usiozidi miaka 45.
  • Awe na vyeti kamili vya mafunzo ya fani aliyosomea (Cheti cha Kidato Cha Nne, Sita na Taaluma aliyosomea.
  1. Elimu kiwango cha kuanzia astashahada na kuendelea ya miamba na madini Geology kutoka vyuo vinavyotambulika.
  2. Awe na nyaraka zote muhimu ikiwemo leseni ya taaluma/kazi kutoka mamlaka husika
  3. Awe na uzoefu usiopungua miaka miwili.

 MAOMBI YOTE YAAMBATANISHWE NA,

  1. Nakala ya cheti cha kuzaliwa.
  2. Nakala ya cheti cha kidato cha nne au/ na cha sita au stashahada kulingana na kada ya mwombaji. Kwa aliyesoma nje ya nchi au mitaala ya nje ya nchi waambatanishe cheti cha ithibati kutoka baraza la mitihani Tanzania (NECTA).
  • Nakala ya vyeti vya Taaluma na Transcript, Aidha waliosoma vyuo vya nje ya nchi, waambatishe cheti cha Ithibati kutoka TCU.
  1. Wasifu (CV).
  2. Picha ndogo (passport size) moja ya hivi karibuni.
  3. Nakala ya kitambulisho cha uraia (NIDA/ Namba ya NIDA).
  • Iwapo majina yako yanatofautiana katika vyeti vyako Pamoja na cheti cha kuzaliwa na NIDA hakikisha unawasilisha kiapo cha majina (Deed Pool) kutoka kwa Msajili wa viapo na kusajiliwa na Msajili wa hati, wizara ya Ardhi na maendeleo ya makazi.

NAMNA YA KUTUMA MAOMBI.

Maombi yote yatumwe ndani ya wiki mbili tangu tarehe ya kutoka kwa Tangazo hili (mwisho wa kutuma maombi ni Tarehe 16/02/2023). Maombi yote yatumwe kwa ofisi ya Katibu Mkuu-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki S.L.P 10 LUSHOTO Au kwa barua Pepe : This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Hits: 355
  1. Tangazo la nafasi ya kazi DAKTARI DARAJA LA II
  2. Mch. Emmanuel Mtoi atambulishwa Usharika wa Kana sasa kuliongoza Jimbo la Pwani.
  3. Askofu Dkt. Mbilu afungua Kanisa na kuweka jiwe la msingi la Madarasa ya Watoto wa Shule ya Jumapili katika Usharika wa Magamba.
  4. Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu aongoza Ibada ya mazishi ya Mch. Sabina Lumwe.

Page 1 of 77

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • ...
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10

Back to Top

© 2023 ELCT North Eastern Diocese