ELCT North Eastern Diocese
TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM
- Details

TANGAZO LA NAFASI YA KAZI
Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya Kilutheri yaliungana na kuunda Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania. Leo hii KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) yenye Makao Makuu yake Wilayani Lushoto Mkoani Tanga ni miongoni mwa Dayosisi 28 za KKKT.
Dayosisi hii inaitwa hivyo kwakuwa inapatikana Kaskazini Mashariki mwa Tanzania katika Mkoa wa Tanga. Kwahiyo KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ni Taasisi ya dini iliyosajiliwa tarehe 19 Juni 1963 na Makao yake Makuu yapo Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga. Dhamira ya KKKT-DKMs ni kufundisha na kuhubiri neno la Mungu na kutoa huduma nzuri za kiroho, kimwili, kiakili, kiuchumi na kijamii kwa watu wote. Taasisi hii inatangaza nafasi moja ya kazi ya MENEJA WA SHAMBA KATIKA KITUO CHAKE CHA IRENTE FARM.
Shamba la Irente Farm lenye ukubwa wa ekari (acres) 507 ni Kituo cha mfano cha kilimo endelevu kinacholenga kuendeleza uzalishaji wa kisasa, kuongeza tija, na kuchangia maendeleo katika Kanisa na jamii kupitia mbinu bora za kilimo na ufugaji. Ili kuimarisha ufanisi na ubora wa huduma zake ikiwemo huduma za Malazi (Hotel/Lodge), Kiwanda Kidogo cha Maziwa na Uzalishaji wa Jam na asali,Mazao ya misitu na nyuki,mikate ya asili ya Irente (Brown bread) ,pamoja na hayo, Irente Farm ni eneo ambalo linatunza uanuwai wa viumbe hai (biodiversity) kwa kuhifadhi miti ya asili hivyo basi Dayosisi inakaribisha maombi kutoka kwa watu wenye sifa stahiki, uadilifu, na moyo wa kuhudumu katika nafasi hii.
Majukumu ya Kazi
- Kusimamia na kuratibu shughuli zote za kilimo na ufugaji katika Kituo cha Irente Farm.
- Kuandaa na kutekeleza mipango ya uzalishaji wa mazao na mifugo kwa ufanisi.
- Kusimamia matumizi sahihi ya rasilimali za shamba ikiwa ni pamoja na wafanyakazi, pembejeo na vifaa.
- Kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu mbinu bora na za kisasa za kilimo na ufugaji.
- Kuandaa na kuwasilisha ripoti za maendeleo ya shughuli za shamba kwa uongozi husika.
- Kushirikiana na wadau mbalimbali katika kukuza na kuendeleza shughuli za kilimo endelevu.
- Kusimamia shughuli zote za hoteli iliyopo ndani ya shamba la Irente Farm
- Kusimamia ufuatiliaji wa taratibu za kisheria za Nchi,afya, Usalama, Mapato na Leseni
Sifa za Mwombaji
Mwombaji anatakiwa kuwa na:
- Shahada ya Kilimo (Agriculture) au Shahada ya Utawala wa Biashara au Taaluma nyinginezo zinazoendana na kazi hiyo kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.
- Uzoefu wa angalau miaka miwili (5) katika usimamizi wa shughuli za kilimo na/au ufugaji.
- Uwezo mzuri wa kutumia kompyuta na kuandaa ripoti za kitaalamu.
- Uwezo wa kufanya kazi kwa kujitegemea na kwa ushirikiano.
- Utayari wa kuishi na kufanya kazi Irente – Lushoto.
- Maadili mema ya Kikristo na moyo wa kuhudumu jamii.
Katibu Mkuu KKKT-DKMs
S.L.P 10,
LUSHOTO TANGA
Kupitia email : This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.
- Barua ya maombi iambatanishwe na nakala za vyeti vya Elimu, Wasifu wa mwombaji (Cv), Cheti cha kuzaliwa, na nakala za vyeti vyote vya ujuzi mbalimbali (kama unavyo).
- Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 20/04/2026 saa 9:59 alasiri
- Waombaji watakaokidhi vigezo ndio watakaoitwa kwenye Usaili (Interview)
- Tarehe ya Usaili watajulishwa kwa njia ya simu/barua pepe.
- Hits: 865
Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji NSSF
- Details

Leo tarehe 01/04/2026, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amepokea ugeni kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika Makao Makuu ya Ofisi za KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Ujumbe huo uliongozwa na Mkurugenzi wa Uendeshaji kutoka makao makuu ya NSSF Dar es Salaam, Ndugu Omary K. Mziya.
Katika mazungumzo yao, pande zote mbili zimejadili kwa kina namna Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, kama mdau muhimu wa maendeleo inavyoendelea kushirikiana vyema na NSSF. Ushirikiano huo umeelezwa kuwa na mchango mkubwa.
Ndugu Omary K. Mziya alieleza kufurahishwa kwake na mapokezi pamoja na mazungumzo yenye tija aliyoyapata kutoka kwa uongozi wa Dayosisi chini ya uongozi wa Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu. Alisisitiza kuwa NSSF itaendelea kushirikiana kwa karibu na Dayosisi ili kuhakikisha malengo ya maendeleo endelevu yanafikiwa.
Kwa upande wake, Askofu Dkt. Mbilu alishukuru ujio wa ugeni huo na kupongeza ushirikiano uliopo, akiahidi kuendelea kuimarisha mahusiano hayo.
- Hits: 850
TAARIFA
- Details

Uongozi wa KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ukiwakilishwa na Katibu Mkuu Mwl. Julius Madiga, umefanya hafla ndogo ya makabidhiano ya mradi wa maji (Mazi kwa Woshe) tarehe 10/03/2026 katika ofisi ya Afisa Tarafa-Mnazi.
Lengo kuu la hafla hiyo lilikuwa ni mkandarasi mjezi wa kampuni ya Ntama and faith company lmtd, kukabidhi rasmi mradi huo kwa Dayosisi, na baadaye Dayosisi kupitia Katibu Mkuu kukabidhi mradi kwa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) pamoja na Kamati ya Maji ya UMBAWASO kwa ajili ya uendeshaji na usimamizi wake.
- Hits: 1379
ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION
- Details

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, leo tarehe 04 Machi 2026, amezindua rasmi Bodi ya Mfuko wa Pension iliyochaguliwa na Halmashauri Kuu ya Dayosisi.
- Hits: 1586
Page 1 of 136

