ELCT North Eastern Diocese
Dean Mstaafu Michael Kanju akabidhi rasmi majukumu ya ofisi ya Msaidizi wa Askofu KKKT-DKMs kwa Dean Mteule Frank Mntangi.
- Details
Dean Mteule Frank Richard Mntangi, ametambulishwa rasmi katika Makao Makuu ya Ofisi ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) yaliyopo Lushoto Tanga. Zoezi hili la utambulisho lililoongozwa na Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu. Dean Mtangi amepokelewa na kutambulishwa kwa wakurugenzi pamoja na watumishi wa Ofisi Kuu.
Dean Mteule Mntangi, akizungumza kwenye Ibada ya asubuhi ya leo tarehe 15/04/2025 ameahidi kutumika kwa uaminifu katika nafasi hiyo na kuahidi kutoa ushirikiano katika idara,vitengo na watenda kazi wote katika Dayosisi ili kufikia malengo,maono na mipango ya Dayosisi.
Kwa upande wake Dean Mstaafu Kanju amemshukuru Askofu Dkt. Mbilu, kwa kumuamini kwa miaka yote aliyokua msaidizi wake kuanzia tarehe 01/12/2020,ametoa shukrani za dhati kwa kurugenzi na watumishi wote wa Ofisi Kuu kwa jinsi walivyomuonyesha ushirikiano,upendo na mshikamano katika kipindi chote cha utumishi wake katika Ofisi ya Msaidizi wa Askofu.
Makabithiano ya ofisi yameanza kufanyika leo tarehe 15/04/2025 na ya taendelea mpaka siku za usoni kutokana na ukubwa na umuhimu wa Kurugenzi ya Misioni na Uinjilisti kama kurugenzi mama katika Dayosisi.
Dean Mteule Mch. Mntangi ataingizwa kazini rasmi tarehe 20/07/2025 katika Usharika wa Kanisa Kuu Lushoto.
- Hits: 263
Mch. Frank Richard Mntangi Dean Mteule KKKT-DKMs
- Details
Wajumbe 217 kati ya 246 wa Mkutano Mkuu wa tano (5) baada ya Jubilee ya miaka 125 ya Injili KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) sawa asilimia 88.5% wamemuidhinisha Mchungaji Frank Richard Mntangi kuwa Msaidizi wa Askofu (Dean Mteule) wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.
Mch. Frank Mntangi ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Jimbo la Pwani, ameteuliwa kuhudumu nafasi hiyo ya msaidizi wa Askofu ambayo kwa sasa inaongozwa na Mch. Michael Mlondakweli Kanju anayestaafu kwa mujibu wa sheria za utumishi za KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.
- Hits: 799
Askofu Dkt. Mbilu ziarani Shule ya Sekondari Lwandai
- Details

- Hits: 1455
Page 1 of 126