ELCT North Eastern Diocese
Toggle Navigation
  • Home
  • Our Diocese
  • Wopa
  • Gallery
  • Institutions
    • Irente Children's Home
    • Irente School for the Blind
    • Rainbow School
    • Lwandai Secondary School
    • Lutindi Mental Hospital
    • Bangala Lutheran Junior Seminary
    • Bumbuli Hospital
    • SEKOMU university
    • Namna ya kuchangia kazi za maendeleo na Vituo vya kutoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu (KKKT-DKMs)
  • Calendar
  • Projects
    • Irente Biodiversity Reserve
    • UTC - Usambara Technological Center
    • Restaurants and Hostels
      • Tumaini Mbuyukenda Hostel and Restaurant
      • Martin Luther Garden and Restaurant
      • Tumaini Songe Restaurant and Hostel
      • Hohen Restaurant and Hostel
      • Tumaini Lushoto Restaurant and Hostel
  • Superintendent
    • Coast Superintendent
    • Northern Superintendent
    • Southern Superintendent
    • Plains Superintendent
  • New-clips
  • Contact us
  • You are here:  
  • Home

Bishop Rev.Dr. Msafiri J. Mbilu

Change Language

English German Spanish Swahili Swedish

News & Updates

  • Ziara ya Askofu Dkt. Mbilu Shule ya Bishop Jali Lutheran Junior Seminary,

    Ziara ya Askofu Dkt. Mbilu Shule ya Bishop Jali Lutheran Junior Seminary,

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Mbi...
  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI YA KAZI Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya...
  • Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji  NSSF

    Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji NSSF

    Leo tarehe 01/04/2026, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amepokea ugeni kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifa...
  • TAARIFA

    TAARIFA

    Uongozi wa KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ukiwakilishwa na Katibu Mkuu Mwl. Julius Madiga, u...
  • ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Dkt. Msafiri Jos...

.



 

 

Staff Email

ELCT North Eastern Diocese

Ziara ya Askofu Dkt. Mbilu Shule ya Bishop Jali Lutheran Junior Seminary,

  • Print
Details
Published: 05 May 2026

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Mbilu, leo tarehe 05/05/2026 amefanya ziara ya kikazi katika Shule ya Bishop Jali Lutheran Junior Seminary, yenye lengo la kukagua na kujionea hali ya miundombinu pamoja na maendeleo ya kitaaluma shuleni hapo.

Akizungumza na walimu na wanafunzi, Askofu Dkt. Mbilu amesisitiza umuhimu wa kuenzi misingi iliyowekwa na viongozi wa Dayosisi waliopita akiwemo Hayati Joseph Mathayo Jali kuendelea kutiana moyo ili kuhakikisha yale yaliyoyanzishwa yanaendelezwa kwa mafanikio zaidi.

Katika hatua nyingine, Askofu Dkt. Mbilu ametoa pole kwa jumuiya ya shule hiyo kufuatia kifo cha aliyekuwa mwalimu mkuu wa shule hiyo Mwl. Mwanga kilichotokea mwaka jana huku akiwahimiza kubaki imara na kuendelea kushirikiana katika kujenga mustakabali wa shule hiyo.

Aidha, Askofu Dkt. Mbilu amewapongeza walimu na wanafunzi kufuatia matokeo mazuri ya kitaaluma, hususani wanafunzi waliofaulu kwa daraja la pili na la tatu, akisisitiza kuwa kwa kuongeza juhudi katika masomo, shule hiyo ina uwezo mkubwa wa kufika mbali zaidi kitaaluma.

Kwa upande wa maendeleo ya miundombinu, Askofu Dkt.Mbilu amesema Dayosisi inaendelea kutafuta njia bora za kuboresha mazingira ya kujifunzia. Pamoja na uwepo wa maji Askofu Dkt. Mbilu ameahidi kusaidia upatikanaji wa maji ya uhakika kwa kununua pampu ya kisima ambacho kishaa chimbwa pamoja na matanki mawili ya kuhifadhia maji ili kuwa na uhakika wa upatikanaji wa maji wakati wote.

Sambamba na hilo, Askofu Dkt.Mbilu ameahidi kulifanyia kazi suala la usafiri kwa kuangalia uwezekano wa kutoa gari moja liliyopo katika Ofisi Kuu ya Dayosisi ili liweze kupelekwa shuleni hapo ndani ya wiki ijayo kwa ajili ya kuwahudumia walimu na wanafunzi.

Katika jitihada za kuboresha elimu ya TEHAMA, Askofu Dkt. Msafiri Mbilu amemuelekeza Afisa TEHAMA, wa Dayosisi Amasia Shemkala, kufuatilia upatikanaji wa kompyuta tano pamoja projector na Printer, ili kuimarisha mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji katika shule husika.

Hatua hii ya Baba Askofu inaonesha kwa vitendo umuhimu mkubwa wa TEHAMA katika sekta ya elimu. Kupitia matumizi ya teknolojia, walimu wanaweza kufundisha kwa njia shirikishi na yenye mvuto zaidi, huku wanafunzi wakipata fursa ya kujifunza kwa vitendo na kujiandaa kukabiliana na mahitaji ya dunia ya kisasa inayotegemea teknolojia.

Aidha, upatikanaji wa vifaa hivi utasaidia kuongeza ufanisi wa ufundishaji, kupanua wigo wa maarifa kwa wanafunzi, na kukuza ubunifu pamoja na stadi za kidijitali ambazo ni muhimu katika soko la ajira la sasa na la baadaye. TEHAMA si nyenzo ya ziada tena, bali ni hitaji la msingi katika kuhakikisha elimu bora na jumuishi inapatikana kwa wote

Katika ziara hii Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, aliambata na Mkurugenzi wa Huduma za Jamii Mwl. Afizai Vuliva.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Huduma za Jamii KKKT-DKMs ametoa shukrani za dhati kwa Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu kufuatia ziara yake katika Shule hiyo ya Bishop Jali Lutheran Junior Seminary, akieleza kuwa uwepo wa kiongozi huyo ni faraja kubwa na chachu ya maendeleo katika taasisi hiyo.

Akizungumza baada ya ziara hiyo, Mkurugenzi huyo amesema kuwa maelekezo na ushauri uliotolewa na Baba Askofu ni ya msingi katika kuboresha huduma za elimu na malezi kwa wanafunzi. Ameahidi kuyafanyia kazi kwa haraka na kwa umakini maelekezo yote yaliyotolewa, ili kuhakikisha shule inaendelea kuwa kituo bora cha malezi, taaluma na nidhamu.

Aidha, amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya uongozi wa Dayosisi na taasisi zake ni nguzo muhimu katika kufanikisha malengo ya kutoa elimu yenye viwango vya juu, akiahidi kuendelea kusimamia utekelezaji wa maagizo hayo kwa ufanisi na uwajibikaji

 

Hits: 358

TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

  • Print
Details
Published: 01 April 2026

TANGAZO LA NAFASI YA KAZI

Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya Kilutheri yaliungana na kuunda Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania. Leo hii KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) yenye Makao Makuu yake Wilayani Lushoto Mkoani Tanga ni miongoni mwa Dayosisi 28 za KKKT.

Dayosisi hii inaitwa hivyo kwakuwa inapatikana Kaskazini Mashariki mwa Tanzania katika Mkoa wa Tanga. Kwahiyo KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ni Taasisi ya dini iliyosajiliwa tarehe 19 Juni 1963 na Makao yake Makuu yapo Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga. Dhamira ya KKKT-DKMs ni kufundisha na kuhubiri neno la Mungu na kutoa huduma nzuri za kiroho, kimwili, kiakili, kiuchumi na kijamii kwa watu wote. Taasisi hii inatangaza nafasi moja ya kazi ya MENEJA WA SHAMBA KATIKA KITUO CHAKE CHA IRENTE FARM.

Shamba la Irente Farm lenye ukubwa wa ekari (acres) 507 ni Kituo cha mfano cha kilimo endelevu kinacholenga kuendeleza uzalishaji wa kisasa, kuongeza tija, na kuchangia maendeleo katika Kanisa na jamii kupitia mbinu bora za kilimo na ufugaji. Ili kuimarisha ufanisi na ubora wa huduma zake ikiwemo huduma za Malazi (Hotel/Lodge), Kiwanda Kidogo cha Maziwa na Uzalishaji wa Jam na asali,Mazao ya misitu na nyuki,mikate ya  asili ya Irente (Brown bread) ,pamoja na hayo, Irente Farm ni eneo ambalo linatunza uanuwai wa viumbe hai (biodiversity) kwa kuhifadhi miti ya asili  hivyo basi Dayosisi inakaribisha maombi kutoka kwa watu wenye sifa stahiki, uadilifu, na moyo wa kuhudumu katika nafasi hii.

Majukumu ya Kazi

  • Kusimamia na kuratibu shughuli zote za kilimo na ufugaji katika Kituo cha Irente Farm.
  • Kuandaa na kutekeleza mipango ya uzalishaji wa mazao na mifugo kwa ufanisi.
  • Kusimamia matumizi sahihi ya rasilimali za shamba ikiwa ni pamoja na wafanyakazi, pembejeo na vifaa.
  • Kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu mbinu bora na za kisasa za kilimo na ufugaji.
  • Kuandaa na kuwasilisha ripoti za maendeleo ya shughuli za shamba kwa uongozi husika.
  • Kushirikiana na wadau mbalimbali katika kukuza na kuendeleza shughuli za kilimo endelevu.
  • Kusimamia shughuli zote za hoteli iliyopo ndani ya shamba la Irente Farm
  • Kusimamia ufuatiliaji wa taratibu za kisheria za Nchi,afya, Usalama, Mapato na Leseni

Sifa za Mwombaji

Mwombaji anatakiwa kuwa na:

  • Shahada ya Kilimo (Agriculture) au Shahada ya Utawala wa Biashara  au Taaluma nyinginezo zinazoendana na kazi hiyo kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.
  • Uzoefu wa angalau miaka miwili (5) katika usimamizi wa shughuli za kilimo na/au ufugaji.
  • Uwezo mzuri wa kutumia kompyuta na kuandaa ripoti za kitaalamu.
  • Uwezo wa kufanya kazi kwa kujitegemea na kwa ushirikiano.
  • Utayari wa kuishi na kufanya kazi Irente – Lushoto.
  • Maadili mema ya Kikristo na moyo wa kuhudumu jamii.

 

Katibu Mkuu KKKT-DKMs
S.L.P 10,
LUSHOTO TANGA
Kupitia email
:  This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

  • Barua ya maombi iambatanishwe na nakala za vyeti vya Elimu, Wasifu wa mwombaji (Cv), Cheti cha kuzaliwa, na nakala za vyeti vyote vya ujuzi mbalimbali (kama unavyo).
  • Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 20/04/2026 saa 9:59 alasiri
  • Waombaji watakaokidhi vigezo ndio watakaoitwa kwenye Usaili (Interview)
  • Tarehe ya Usaili watajulishwa kwa njia ya simu/barua pepe.

 

Hits: 1960

Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji NSSF

  • Print
Details
Published: 01 April 2026

Leo tarehe 01/04/2026, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amepokea ugeni kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika Makao Makuu ya Ofisi za KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Ujumbe huo uliongozwa na Mkurugenzi wa Uendeshaji kutoka makao makuu ya NSSF Dar es Salaam, Ndugu Omary K. Mziya.

Katika mazungumzo yao, pande zote mbili zimejadili kwa kina namna Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, kama mdau muhimu wa maendeleo inavyoendelea kushirikiana vyema na NSSF. Ushirikiano huo umeelezwa kuwa na mchango mkubwa.

Ndugu Omary K. Mziya alieleza kufurahishwa kwake na mapokezi pamoja na mazungumzo yenye tija aliyoyapata kutoka kwa uongozi wa Dayosisi chini ya uongozi wa Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu. Alisisitiza kuwa NSSF itaendelea kushirikiana kwa karibu na Dayosisi ili kuhakikisha malengo ya maendeleo endelevu yanafikiwa.

Kwa upande wake, Askofu Dkt. Mbilu alishukuru ujio wa ugeni huo na kupongeza ushirikiano uliopo, akiahidi kuendelea kuimarisha mahusiano hayo.

Hits: 1723

TAARIFA

  • Print
Details
Published: 10 March 2026

Uongozi wa KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ukiwakilishwa na Katibu Mkuu Mwl. Julius Madiga, umefanya hafla ndogo ya makabidhiano ya mradi wa maji (Mazi kwa Woshe) tarehe 10/03/2026 katika ofisi ya Afisa Tarafa-Mnazi.

Lengo kuu la hafla hiyo lilikuwa ni mkandarasi mjezi wa kampuni ya Ntama and faith company lmtd, kukabidhi rasmi mradi huo kwa Dayosisi, na baadaye Dayosisi kupitia Katibu Mkuu kukabidhi mradi kwa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) pamoja na Kamati ya Maji ya UMBAWASO kwa ajili ya uendeshaji na usimamizi wake.

Hits: 2261

Read more ...

  1. ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION
  2. Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika
  3. Askofu Dkt. Mbilu afungua Kikao Kazi cha Tathmini ya Mwaka 2025
  4. Askofu Dkt. Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Helga Walter

Page 1 of 137

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • ...
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10

Back to Top

© 2026 ELCT North Eastern Diocese