ELCT North Eastern Diocese
Toggle Navigation
  • Home
  • Our Diocese
  • Wopa
  • Gallery
  • Institutions
    • Irente Children's Home
    • Irente School for the Blind
    • Rainbow School
    • Lwandai Secondary School
    • Lutindi Mental Hospital
    • Bangala Lutheran Junior Seminary
    • Bumbuli Hospital
    • SEKOMU university
    • Namna ya kuchangia kazi za maendeleo na Vituo vya kutoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu (KKKT-DKMs)
  • Calendar
  • Projects
    • Irente Biodiversity Reserve
    • UTC - Usambara Technological Center
    • Restaurants and Hostels
      • Tumaini Mbuyukenda Hostel and Restaurant
      • Martin Luther Garden and Restaurant
      • Tumaini Songe Restaurant and Hostel
      • Hohen Restaurant and Hostel
      • Tumaini Lushoto Restaurant and Hostel
  • Superintendent
    • Coast Superintendent
    • Northern Superintendent
    • Southern Superintendent
    • Plains Superintendent
  • New-clips
  • Contact us
  • You are here:  
  • Home

Bishop Rev.Dr. Msafiri J. Mbilu

Change Language

English German Spanish Swahili Swedish

News & Updates

  • Askofu Dkt. Mbilu afungua Kikao Kazi cha Tathmini ya Mwaka 2025

    Askofu Dkt. Mbilu afungua Kikao Kazi cha Tathmini ya Mwaka 2025

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Jos...
  • Askofu Dkt. Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Helga Walter

    Askofu Dkt. Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Helga Walter

    Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Mbilu, alipata fursa ya kupokea ugeni w...
  • Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Halmashauri Kuu KKKT-DKMs

    Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Halmashauri Kuu KKKT-DKMs

    Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Halmashauri Kuu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania – Dayosi...
  • Askofu Dkt. Mbilu aweka wakfu pikipiki rasmi kutumika Idara ya Mashamba

    Askofu Dkt. Mbilu aweka wakfu pikipiki rasmi kutumika Idara ya Mashamba

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Jos...
  • Askofu Dkt. Mbilu Aongoza Kikao Kazi cha Wachungaji

    Askofu Dkt. Mbilu Aongoza Kikao Kazi cha Wachungaji

    Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ameongoza kikao kazi cha W...

.



 

 

Staff Email

ELCT North Eastern Diocese

Askofu Dkt. Mbilu afungua Kikao Kazi cha Tathmini ya Mwaka 2025

  • Print
Details
Published: 12 February 2026

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amefungua rasmi kikao cha tathmini kwa kazi zilizotekelezwa katika kipindi cha mwaka 2025.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho kilichofanyika tarehe 12/02/2026 katika Hoteli ya Tumaini Mbuyukenda, Jijini Tanga, Askofu Dkt. Mbilu amesema kuwa lengo kuu la kikao hicho ni kuweka msingi imara kwa watumishi kutambua walipotoka, walipo na wanakoelekea katika utendaji wao wa kazi. Amesisitiza kuwa tathmini ni nyenzo muhimu katika kupima mafanikio, kubaini changamoto na kupanga mikakati madhubuti ya kuboresha utendaji kwa siku zijazo.

Aidha, Askofu Dkt.Mbilu ameeleza kuwa kikao hicho ni semina elekezi yenye dhima ya kujengeana uwezo wa kujitathmini, kujikosoa na kujirekebisha pale panapohitajika. Ameongeza kuwa kupitia semina hiyo, washiriki watapata fursa ya kukumbushana wajibu wao pamoja na kuongeza bidii katika utekelezaji wa majukumu ili kupunguza changamoto na kufikia malengo yaliyowekwa.

Katika hotuba yake ya ufunguza, Askofu Dkt. Mbilu ametoa pongezi kwa watumishi kwa utendaji mzuri wa kazi katika maeneo mbalimbali ndani ya Dayosisi, akisema mafanikio yaliyopatikana ni matokeo ya ushirikiano, uwajibikaji pamoja na kujituma.

Hata hivyo, amesisitiza umuhimu wa kutekeleza kwa vitendo Kauli Mbiu ya Dayosisi ya “Kasi Tofauti”, akitaka ionekane wazi katika utendaji wa kila siku. Amefafanua kuwa kasi hiyo inapaswa kuambatana na Uwazi, kuzingatia Viwango vinavyotakiwa, pamoja na Umakini katika utekelezaji wa majukumu, ikiwemo utoaji wa taarifa sahihi katika ngazi zote ndani ya Dayosisi.

Kwa ujumla, kikao hicho cha tathmini kinatarajiwa kuwa chachu ya maboresho zaidi katika utendaji kazi, huku kikilenga kuimarisha uwajibikaji na kuongeza ufanisi kwa manufaa ya Dayosisi na jamii kwa ujumla.

Tufuatilie kwenye mitandao yetu ya kijamii

INSTAGRAM - / elctned

FACEBOOK ACCOUNT North Eastern Diocese

FACEBOOK PAGE - ELCT-North Eastern Diocese

YOUTUBE - / KKKT DKMS Online TV

WEBSITE: www.elctned.org

KWA MAONI NA USHAURI:

Simu : +255 743 399 798

 

Hits: 36

Askofu Dkt. Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Helga Walter

  • Print
Details
Published: 05 February 2026

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Mbilu, alipata fursa ya kupokea ugeni wa kiongozi wa undugu Helga Walter kutoka Hainberg-Gymnasium Göttingen  nchini Ujerumani. 

Katika mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki tarehe 05/02/2026  , pande zote mbili zilijadili kwa kina namna ya kuendelea kuimarisha na kuboresha undugu uliopo kati yao, hususani katika nyanja za elimu na huduma za kijamii.

Aidha, Askofu Dkt. Mbilu alitumia fursa hiyo kutoa shukrani za dhati kwa Helga pamoja na wadau wengine wa maendeleo kutoka Hainberg-Gymnasium Göttingen kwa michango yao ya kimaendeleo, hususani katika Shule ya Sekondari Lwandai pamoja na vituo vya diakonia vilivyopo Irente vinavyomilikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.

Ziara hiyo ilionesha mshikamano na dhamira ya pamoja ya kuendeleza ushirikiano wenye tija kwa manufaa ya jamii.

Hits: 392

Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Halmashauri Kuu KKKT-DKMs

  • Print
Details
Published: 29 January 2026

 

Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Halmashauri Kuu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) kilichofanyika  tarehe 29 Januari 2026 katika Ukumbi Mdogo wa Mikutano, Utondolo – Lushoto. Kikao hicho kimewakutanisha wajumbe wa Kamati ya Utendaji kwa ajili ya kujadili na kufanya maamuzi muhimu yanayohusu uendeshaji na maendeleo ya D

Hits: 1023

Read more ...

Askofu Dkt. Mbilu aweka wakfu pikipiki rasmi kutumika Idara ya Mashamba

  • Print
Details
Published: 28 January 2026

 

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ameongoza Ibada ya kuweka  wakfu chombo cha usafiri (pikipiki) na kumkabidhi kadi ya pikipiki pamoja na ufunguo Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uchumi, Mipango na Maendeleo, Bi. Pendo Lauwo, kwa ajili ya shughuli za kikazi za kila siku za Idara ya Mashamba.

Ibada hiyo pamoja na makabidhiano hayo yamefanyika tarehe 28/01/2025 katika Ofisi za Makao Makuu ya Dayosisi, Lushoto-Tanga. Chombo hiki cha usafiri kitasaidia katika mazingira ambayo hakuna barabara zinazofikika kwa kutumia usafiri wa gari.

Hits: 1006

Read more ...

  1. Askofu Dkt. Mbilu Aongoza Kikao Kazi cha Wachungaji
  2. TUZO YA PONGEZI KWA KUCHANGIA DENI LA DAYOSISI
  3. Heri ya Mwaka Mpya 2026
  4. Askofu Dkt. Mbilu Akabidhi Gari 1 kwa Kituo Cha Lutindi Mental Hospital

Page 1 of 135

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • ...
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10

Back to Top

© 2026 ELCT North Eastern Diocese