
Kikao cha tathmini ya kazi za Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMS) ambacho kimeanza kufanyika leo hii tarehe 6-9/01/2021 kimefunguliwa na Dean Mteule Mch Michael Kanju kwa niaba ya Askofu Mteule Mch Msafiri Joseph Mbilu ambaye katika utangulizi wa semina hii alisoma neno kuu la mwaka KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kutoka kitabu cha Zaburi: 32:8 “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea;Nitakushauri, Jicho langu likikutazama”.
Malengo ya kikao hiki ni kuweka vipaombele vya Dayosisi kwa mwaka 2021



