
Kikao hiki kilifanyika kwa dhumuni la kumtambulisha Mkurugenzi wa Uchumi Mipango na Maendeleo Bibi. Pendo Lauwo kwa wakuu wa Idara pamoja na wakuu wa vituo vya uzalishaji. Baada ya utambulisho mkurugenzi alipata muda wa kueleza mikakati yake katika utekelezaji wa shughuli za kituo na wakuu wa Idara na vituo walitoa taarifa zao miezi mitatu. Kikao hiki kilifanyika tarehe 15/06/2023 katika ukumbi wa mikutano Utondolo.






