Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs), Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ambaye pia ni msimamizi Mkuu wa mali za Dayosisi amesaini Mkataba wa Makubaliano (MoU) kati ya Chuo cha Kolowa Technical Training Institute (KOTETI) kinacho milikiwa na KKKT-DKMs na Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), makubaliano yanayolenga kuboresha na kukuza taaluma na tafiti katika vyuo hivyo.

KATIKA PICHA:Mkutano wa Maaskofu wote wa CCT na TEC uliofanyika Jijini Dar Es Salaam kwenye kituo cha Baraza la Maaskofu Catholic Tanzania tarehe 11-12/02/2025. Huu ni Mkutano wa Kitaifa wa CSSC (Christian Social Services Commission) ambao ulikuwa na mada Kuu ya kutathmini na kuona jinsi ya kuwa na mpango endelevu wa utoaji huduma bora za Elimu na Afya zinazotolewa na Makanisa nchini (Sustaining the provision of Quality Education and Health Care Services by the Churches in Tanzania).Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ni mmoja wa maaskofu walioshiriki mkutano huu.

 HABARI KWA UFUPI

Wakristo wamekumbushwa kuendelea kumtumaini na kumtegema Mungu pale wanapo pata mafanikio katika maisha yao kwani katika dunia ya sasa wapo waliofanikiwa na mara baada ya kupata mafanikio hayo wakamsahau Mungu na kufuata njia zao, na kuamini kuwa mafanikio hayo wameyapata kwa nguvu zao.

Ufunuo 14:13“Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao”.
 
KATIKA PICHA:Ibada ya mazishi ya Bibi. Elise David Ngome, iliyofanyika leo tarehe 28/01/2025 katika Jimbo la Kusini Usharika wa Mgwashi na kuongozwa na msaidizi wa Askofu KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch. Michael Mlondakweli Kanju akishirikiana na Mkuu wa Jimbo la Kusini Mch. Issai Mweta.