Uncategorised
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu yupo katika ziara ya kikazi Nchini Ujerumani ambapo ameambatana na Dean Mteule Frank Mtangi pia wamepata wasaa wa kutembelea Jimbo la Staaken kwenye Jiji la Berlin.

Askofu Dkt Mbilu aliongoza Ibada ya Jumapili ya tarehe 27/04/2025, ziara hii ya kikazi imekua na vikao mbalimbali vya kuimarisha urafiki na umoja katika kuleta maendeleo chanya ya KKKT-DKMs. Katika kikao hiki Jimbo la Staaken limeamua kuweka nguvu kubwa katika kusaidia Kituo cha Watoto yatima Irente.

Askofu Dkt. Mbilu na Dean Mteule Mntangi wapo katika Mji wa Hannover kushiriki Sikukuu ya Kanisa inayoitwa kwa Kijerumani Kirchentag. Sikukuu hii ya Kanisa la Kiinjili Ujerumani inahudhuriwa na Wakristo wengi sana,na watu 100,000 walishiriki katika Ibada ya Ufunguzi. Sikukuu hii ya Kanisa ilianza tangia tarehe 30/04/2025 hadi tarehe 4/5/2025 Hannover Ujerumani.
Ibada ilipambwa na kikundi cha Tarumbeta cha wapigaji wapatao 3000 na Waimbaji 1200 na Mgeni Rasmi alikuwa Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier ambapo mara baada ya Ibada hiyo Askofu Dkt. Mbilu alipata nafasi ya kufanya mazungumzo na Rais wa Ujerumani kuhusu Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.

- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs), Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amepongeza kazi nzuri inayofanywa na Halmashauri ya Katiba ya KKKT, juu ya zoezi linaloendelea la kuchukuwa maoni juu ya Katiba Mpya ya KKKT na kusema kuwa anaamini Katika Mpya ya KKKT, itakuwa jumuishi na italeta umoja wa kweli katika Kanisa.

- Details
Dean Mteule Frank Richard Mntangi, ametambulishwa rasmi katika Makao Makuu ya Ofisi ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) yaliyopo Lushoto Tanga. Zoezi hili la utambulisho lililoongozwa na Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu. Dean Mtangi amepokelewa na kutambulishwa kwa wakurugenzi pamoja na watumishi wa Ofisi Kuu.
Page 1 of 115