Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameendelea na ziara yake ya kutembelea Jimbo la Pwani na Sharika zake ambapo tarehe 20/04/2024 ametembelea Usharika Mteule wa Lugongo na kuongoza Ibada ya Shukrani.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch.Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amehitimisha ziara yake ya siku tatu ya kutembelea Jimbo la Pwani na Sharika zake kwa kuongoza Ibada ya Jumapili katika Usharika wa Maramba katika Jimbo la Pwani.

Rais wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF) Askofu Henrik Stubkjær ameungana na Watanzania katika kuadhimisha siku ya ugonjwa wa Hemophilia Duniani ambapo jamii imeaswa  kupima mara kwa mara ili kuweza kujua hali ya Afya zao na kuchukua hatua mapema.

 

Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Askofu Dkt. Alex Malasusa amesema kuwa ujio wa Rais wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF), nchini Tanzania Askofu Henrik Stubkjær utaendelea kuimarisha uhusiano uliopo na Makanisa ya Kilutheri  duniani katika kulitangaza neno la Mungu.