Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch. Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amewashukuru Washarikwa wa Usharika wa Mlalo na wana KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kwa namna wanavyojitoa katika kumtumikia Mungu.

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ameupongeza uongozi wa Taasisi ya Elimu ya Kolowa Technical Training Institute (KOTETI), kwa kazi nzuri inayofanyika katika nyanja ya mafunzo kwa kuzingatia kasi na viwango katika utoaji wa Elimu katika taasisi hiyo inayomilikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.

Usharika  Mpya wa Bethania ni Usharika uliozaliwa kutoka katika Usharika Mama wa Kange. Usharika huu uliopo katika Jimbo la Pwani unaundwa na Mitaa miwili ambayo ni Mtaa wa SENTA pamoja na Mtaa wa PENUEL. Mtaa wa Senta upo katika maeneo ya Kange kasera karibu na Chuo cha Utumishi wa Umma na Mtaa wa Penuel upo katika maeneo ya Kasera. Mitaa yote hii miwili ilikua chini ya uangalizi wa Usharika mama wa Kange.

Mkuu wa Shirika la Michaeliskloster lililoko Hildesheim, Hannover nchini Ujerumani, Mch. Prof. Jochen Arnold ameitembelea KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,ambapo ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake na leo tarehe 15/06/2024 akiwa katika Chuo cha Biblia Vuga na kutoa zawadi ya Keyboard nzuri ili isaidie mafunzo ya kozi ya muziki inayotolewa Chuoni hapo.