Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amekutana na kufanya mazungumzo na Wanafunzi wa kozi ya Masters ya Kimataifa ya Usimamizi/Uongozi wa Diakonia ambao wameitembelea Dayosisi yetu kama sehemu yao ya mafunzo kwa njia ya vitendo.

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amefanya Ziara ya kikazi nchini Philippines, kuanzia tarehe 15/5/2024 hadi tarehe 05/06/2024, Ziara hii iliyowezeshwa na chama Cha kiinjili Cha kimisioni, United Evangelical Mission (UEM) imekuwa na malengo ya kumuwezesha Baba Askofu kuhudhuria Makongamano mbalimbali ya Kimisioni katika Chuo Kikuu cha Silliman kilichopo katika Jiji la Dumaguete Mkoa wa Negros Oriental.

Ufunuo 14:13“Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao”.

Katibu Mkuu wa KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mwl. Julius Madiga kwa niaba ya Uongozi wa KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, anasikitika kutangaza kifo cha Bitrice David Mmbali kilichotokea  tarehe 27/05/2024 katika Hospitali ya Mloganzila iliyopo Jijini Dar Es Saalam alipokuwa anapatiwa matibabu.

Matukio katika Picha Ibada ya Mazishi ya Marehemu, Mchungaji Daniel Elierehema Kilangilo Magogo.Mchungaji Mstaafu Daniel Magogo aliitwa mbinguni tarehe 16/05/2024 na tarehe 20/05/2024 imefanyika Ibada ya mazishi yake Iliyoongozwa na Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania,Baba Askofu Dkt. Alex Gehaz Malasusa. na mwili wa marehemu Mchungaji Mstaafu Magogo, umepumzishwa katika makaburi ya familia yaliyopo Kwesimu Lushoto.
  
KATIKA HISTORIA
KUZALIWA: - Marehemu Mch. Daniel Elierehema Kilangilo Magogo alizaliwa tarehe 16/09/1925. ELIMU YA MSINGI: - Alianza elimu ya msingi mwaka 1944 katika Shule ya Msingi Lushoto Extended Primary School. MIDDLE SCHOOL: - Alisoma Vugiri Middle School mwaka 1948 – 1951. KUBATIZWA: - Alibatizwa mwaka 1950 akiwa na miaka 25. ELIMU YA SEKONDARI: - Alisoma Tanga School mwaka 1952 hadi 1953.