Leo tarehe 10/01/2021 Askofu Mteule Mch Dkt Msafiri Joseph Mbilu mara baada ya Ibada katika Usharika wa Kana Jimbo la Pwani,amepata nafasi ya kufanya kikao na baadhi ya wazee wa Kanisa na Wazee maarufu wa Jimbo la Pwani. Kikao kilifanyika katika hostel ya Mbuyu Kenda Tanga lengo likiwa ni kupata maoni ya wazee hao juu ya namna bora ya kuiendeleza na kuiimarisha hostel ya Mbuyukenda.