Rais wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (Lutheran World Federation “LWF”), Askofu Henrik Stubkjær amewasili nchini Tanzania tayari kuanza ziara yake ya siku 3 ya kuitembelea KKKT,ambapo amepokelewa na  na mwenyeji wake Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania  (KKKT) Askofu Dkt. Alex Gehaz Malasusa .

 
Ufunuo 14:13 “Nikasikia sauti kutoka Mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao”

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, kwa niaba ya Halmashauri Kuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki  ametangaza uteuzi na mabadiliko madogo ya Wakuu wa Majimbo.Hii ni mara baada ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Dayosisi kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano Utondolo Lushoto Tarehe 26-27/03/2024.

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,Mch Dkt Msafiri Joseph Mbilu, amewataka Vijana wa UKWATA Mkoa wa Tanga, kukubali kulelewa kiroho na kuwa mfano wa kuigwa wawapo shuleni kwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo  kwa kufuata maadili mema na kuwa mstari wa mbele katika ufaulu mzuri darasani.