Uncategorised
- Details
Mei 9 mwaka 2021 ilikuwa ni siku iliyotawaliwa na nderemo, vifijo na shamrashamra katika viunga vya Lushoto, siri nyuma ya furaha hii si nyingine bali ni historia mpya kuandikwa, wakristo wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki walipata Askofu mpya, kiongozi ambae atayabeba maono na dira ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki huyu sio mwingine bali ni Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu.


Askofu Dkt. Mbilu licha ya kusimamia Dayosisi kupitia kauli mbiu yake ya kasi tofauti, ameendelea kuwa mnyenyekevu na msikivu kwa washarika wote kwani anaamini ushirikiano mzuri wanaompa ndio msingi wa mafaniko ya Dayosisi.




- Details


- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, anaendela na ziara yake ya kikazi iliyoanza tarehe 26/04/2024 nchini Marekani katika Mji wa Philadelphia, ambako ndiko Makao Makuu ya Synod rafiki ya Southeastern Pennsylvania yalipo. Hii ni mojawapo ya Synod za Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Marekani.
- Details

Mchungaji Jeremia Mboko wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Jimbo la Pwani Usharika wa Mikanjuni amewashukuru na kuwapongeza waumini wa Usharika huo ambao wanaendelea kujitoa katika kuchangia deni linalo ikabili Dayosisi huku akiwataka washarika wote kuingia kazini kikamilifu katika kuchangia deni hilo.
Page 29 of 124

