Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amemshukuru Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Askofu Dkt. Alex Gehaz Malasusa pamoja na Halmashauri Kuu ya KKKT kwa kuja na mpango wa pamoja kwa Dayosisi zote 28 za KKKT kuchangia kulipa deni linaloikabili KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs).
Msaidizi wa Askofu KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mchungaji Michael Mlondakweli Kanju, amewataka Wakristo kujenga moyo wa kujitoa kwa mali,sadaka kwa ajili ya Kristo na Kanisa lake, kwani ipo siri kubwa ya kufanikiwa kwa kujitoa katika kumtumikia Mungu.

HABARI KWA UFUPI TANGA

HABARI KWA UFUPI
Ibada ya Jumapili siku ya Bwana ya 9 baada ya utatu aliyofanyika KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Jimbo la Pwani Usharika wa Pongwe Mtaa wa Diary tarehe 28/07/2024. Ibada ilikuwa na matendo makuu mbalimbali ikiwemo uwekwaji wa Jiwe la Msingi la Kanisa Pamoja na Harambee ya Ujenzi wa Kanisa la Mtaa huo.
HABARI KWA UFUPI:
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amewakumbusha Wakristo kuishi maisha ya kumpendeza Mungu ili wawe na mwisho mwema. Askofu Dkt.Mbilu ametoa wito huo katika Ibada ya Mazishi ya Marehemu Mzee Dastan Mazimu yaliyofanyika katika Usharika wa Bumbuli tarehe 27/07/2024.