Msaidizi wa Askofu toka KKKT Dayosisi ya Karagwe , Mch Yared A. Wakami yupo ziarani KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ambapo leo tarehe 14/06/2021 ametembelea ofisi za wakuu wa majimbo ya Pwani na Tambarare.

Mchungaji Thadeus A. Ketto ameingizwa kazini kuwa Mkuu wa Jimbo la PWANI KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ikumbukwe katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Dayosisi kilichofanyika tarehe 26/11/2020 kilimchagua Mchungaji Thadeus A. Ketto kuwa Mkuu wa Jimbo kwa kufuata Kanuni ya VIII ya Katiba  ya KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.

Askofu Dkt Msafiri Joseph Mbilu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki  leo tarehe 12/06/2021 ameweka jiwe la msingi katika Usharika wa Kange mtaa wa Maweni.

Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amewashukuru walimu pamoja na wafanya kazi wa vituo vya Irente Rainbow School,Irente School for the Blind, pamoja na kituo cha Irente Children’s Home kwa namna wanavyoendelea kuwahudumia watoto katika vituo hivyo.