“……Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.”

Leo tarehe 07/11/2021 imekuwa siku ya baraka kwa washarika wa Usharika wa Kana, Jimbo la Pwani, ambapo vijana wapatao 33 walibarikiwa na mmoja kati yao alibatizwa.

"Naye atafuta kila chozi katika macho yao,wala mauti haitakuwepo tena,wala kilio, wala maumivu hayatakuwepo tena, kwa kuwa mambo ya kwanza  yamekwisha kupita " UFUNUO 21:4.

 Kaimu Katibu Mkuu wa KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Godfrey Tahona Walalaze kwa niaba ya Uongozi wa KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki anasikitika kutangaza kifo cha Mama Mzazi wa  Mch.Juliana Mahundo, Bi. Raheli Mahundo, kilichotokea  tarehe 05/11/2021.

 Ibada ya mzishi itafanyika siku ya Jumatatu tarehe 08/11/2021katika mtaa wa Mindu, Usharika wa Kwabada-Muheza.

 Uongozi unatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki popote pale walipo. BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe.

 

 

TANZIA

 

"Naye atafuta kila chozi katika macho yao,wala mauti haitakuwepo tena,wala kilio, wala maumivu hayatakuwepo tena, kwa kuwa mambo ya kwanza  yamekwisha kupita " UFUNUO 21:4.

 Kaimu Katibu Mkuu wa KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Godfrey Tahona Walalaze kwa niaba ya Uongozi wa KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki anasikitika kutangaza kifo cha Baba Mzazi wa  Mch. Lemmy Baruti, Mzee Tamilwai Augustino Baruti kilichotokea usiku wa tarehe 31/10/2021 katika hospitali ya Wilaya ya Pangani.

 Taratibu za mazishi zinaendelea na mtajulishwa.

 Uongozi unatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki popote pale walipo. BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe.

 

...........                ................                    .................                      .....................

 

 

Leo tarehe 31/10/2021 imekuwa siku ya baraka kwa washarika wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Usharika wa Irente Jimbo la Kusini ambapo vijana wapatao 24 walipata kipaimara.