Leo tarehe 30/10/2021 Imekuwa siku ya baraka tele kwa washarika wa Usharika wa Hale Jimbo la Tambarare kwani vijana wapatao 164 walipata kipaimara na sita 6 kati yao walibatizwa.

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Mashariki na Pwani Mch Dkt. Alex Malasusa amewakumbusha waimbaji kuwa uimbaji unamchango mkukwa katika kumuita mtu kwa mungu na uimbaji umetumika kama chombo cha uinjilisti hivyo kukuwa kwa injili katika KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki na sehemu nyingine upo mchango mkubwa wa waimbaji.

Ikiwa ni mara ya kwanza tangu Kuchaguliwa na Kuingizwa kazini kuiongoza KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amewashukuru washarika wa Usharika wa Mkata kwa namna wanavyoendelea kumtumikia Mungu.

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amewapongeza washarika wa Usharika wa Mkata Mtaa wa Magamba kwa kazi kubwa na nzuri ya ujenzi wa Kanisa unaoendelea.


Pongezi hizo amezitoa leo tarehe 22/10/2021, alipokuwa anaongoza Ibada ya uwekwaji wa Jiwe la Msingi, Katika Usharika wa Mkata Mtaa wa Magamba.


Mtaa huo wa Magamba ulianzishwa mwaka 2012 ukiwa na waumini saba na sasa unajumla ya waumini 54.