Uncategorised
- Details

Kaimu katibu Mkuu Mch. Godfrey T. Walalaze leo tarehe 05/02/2021 amehitimisha Semina elekezi ya mafunzo ya kuimarisha Vituo vya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki iliyo anza jana Katika ukumbi wa mikutano Cathedral ambapo amegusia mambo mbalimbali ikiwemo umuhimu wa kuzijua Kanuni, Sheria na Taratibu za Kazi.
- Details
Idara ya Jinsia na Watoto KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki imepata uongozi mpya ambao umechaguliwa kuiongoza idara hiyo kwa miaka minne ijayo walio chaguliwa ni Bi. Christina Peter ambaye amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Idara, Bi. Mercy Mushi, Makamu Mwenyekiti, Bi. Miriam Mndeme, Mwandishi na Bi. Flora Luziga, Mhazini.

(KATIKA PICHA NI) Mratibu wa Idara ya Jinsia na Watoto KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Happyness Diu wa pili kulia akiwa na Viongozi wapya, Bi. Flora Luziga wa kwanza kushoto, Bi. Mercy Mushi wa pili kutoka kushoto, Bi. Christina Peter wa tatu toka kushoto (Mwenyekiti wa Idara) na Bi. Miriam Mndeme wa kwanza kulia.
Kwa niaba ya Uongozi huo mpya Mwenyekiti wa Idara Bi. Christina Peter amewashukuru wajumbe wa mkutano huo kwa imani kubwa kwao na kuahidi kufanya kazi hiyo kwa maslahi mapana ya Dayosisi na Kanisa kwa Ujumla.
- Details

Leo tarehe 28 Januari kumefanyika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Idara ya Jinsia na Watoto KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Ufunguzi huu ulifanywa na Askofu Mteule, Mch. Dkt. Msafiri Joseph Mbilu .Mkutano huu unafanyikia katika Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa (SEKOMU). Katika hotuba yake ya Ufunguzi Askofu Mteule alitoa wito kwa Idara hii kufikiri juu ya miradi mbalimbali.Aidha Askofu Mteule amewahakikishia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Idara ya Jinsia na Watoto kuwa ofisi ya Dayosisi anayoiongoza iko tayari kushirikiana na idara na kushauri juu ya mawazo yoyote ya kuanzisha miradi.
- Details


Askofu Mteule wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch. Dkt Msafiri Joseph Mbilu pamoja na viongozi wengine wa Dayosisi wameshiriki Mazishi ya Baba mzazi wa Prof . Christopher Mahonge (Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa-SEKOMU) yaliyofanyika katika Kijiji cha Vuga, Lushoto leo tarehe 20/01/2021. Marehemu Mzee Paulo Mahonge enzi za uhai wake aliitumikia Lutheran Junior Seminary kwa miaka mingi.
Page 120 of 125

