Uongozi wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, unatoa pole kwa Baba Askofu Dkt. Fredrick Onael Shoo Mkuu wa KKKT na Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini,kufuatia kifo cha Askofu Mstaafu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini, Dkt. Erasto Kweka, kilichotokea tarehe:25/11/2023.

Uongozi unatoa pole kwa familia, Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Dayosisi ya Kaskazini ,Wakuu wa Majimbo wa Dayosisi ya Kaskazini, Wakuu wa Idara zote  za Dayosisi Wachungaji wote wa Dayosisi ya Kaskazini pamoja na  Washarika wote wa Dayosisi ya Kaskazini.

 BWANA ametoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe.

Askofu wa KKKT -Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, Tarehe 24 / 11 / 2023 ameanza ziara yake ya Kikazi Katika Jimbo la Tambarare Usharika wa Mtonga na kuongoza Ibada zilizokuwa na matendo mbalimbali ikiwemo uwekaji wa jiwe la ufungizi wa Kanisa Mtaa wa Ngua,Ibada ya kuweka jiwe la msingi la Kanisa Mtaa wa Tabora, Ibada ya kuwabariki Vijana wa Kipaimara katika Mtaa wa Sayuni na ufunguzi wa Kongamano la ITA NAE ATAITIKA linalofanyika katika Senta ya Usharika wa Mtonga.

 
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amewataka wanafunzi wa Chuo cha Biblia Vuga kuendelea kufuata mafundisho yenye mafafanuzi sahihi wanayoyapata Chuoni hapo yanayozingatia taratibu na misingi ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT).
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ameongoza Ibada ya Jumapili ya tarehe 19/11/2023 katika Jimbo la Kusini, Usharika wa Ngulwi B ambapo kulikua na tendo la Kipaimara ambapo vijana wapatao 108 walibarikiwa na watatu kati yao kubatizwa.