MATUKIO KATIKA PICHA:- Tarehe 22/10/2023 ilikuwa siku ya furaha na baraka tele kwa washarika wa Jimbo la Kusini Usharika wa Manka ambapo, Jumla ya Vijana wa Kipaimara 60 wamebarikiwa katika Jimbo la Kusini Usharika wa Manka huku Vijana hao wakitoa shukrani zao kwa Baba Askofu Dkt Msafiri Joseph Mbilu kwa kupata nafasi ya kufundishwa mafundisho ambayo yameimarisha Imani yao huku wakisema kupitia mafundisho hayo mazuri ya neno la Mungu wamepata msingi imara wa kiroho na kimwili.

 

MATUKIO KATIKA PICHA. Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu akiwa katika Ibada ya kuwabariki Vijana wa Kipaimara katika Jimbo la Kusini, Usharika wa Bungu,Ibada hii ilitanguliwa na ufunguzi wa Makanisa katika Mtaa wa Kwakibomi pamoja na Mtaa wa Msasa huku Jumla ya Vijana 127 wakibarikiwa na wawili kati yao kubatizwa.

MATUKIO KATIKA PICHA: Harambee ya kuchangia kazi za maendeleo na vituo vinavyotoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalum (Diakonia) kwa Dini zote vinavyomilikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, iliyofanyika tahere 15/10/2023, katika ukumbi wa Regal Naivera Tanga.

KATIKA PICHA: Ibada ya Jumapili ya tarehe 15/10/2023 kutoka Jimbo la Tambarare Usharika wa Muheza. Ibada hii iliongozwa na Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ilikuwa na tendo la kuwabariki vijana wa Kipaimara. Pamoja na hayo Vijana hao waliobarikiwa wamemshukuru Mhashamu Baba Askofu Dkt. Msafiri Mbilu kwa kufundishwa neno la Mungu kwa kipindi cha miaka miwili huku wakitoa pongezi kwa kazi mbalimbali za maendeleo zinazofanyika ndani ya Dayosisi chini ya uongozi wa Baba Askofu Dkt. Mbilu.