Mchungaji Jeremia Mboko wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Jimbo la Pwani Usharika wa Mikanjuni amewashukuru na kuwapongeza waumini wa Usharika huo ambao wanaendelea kujitoa katika kuchangia deni linalo ikabili Dayosisi huku akiwataka washarika wote kuingia kazini kikamilifu katika kuchangia deni hilo.

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameendelea na ziara yake ya kutembelea Jimbo la Pwani na Sharika zake ambapo tarehe 20/04/2024 ametembelea Usharika Mteule wa Lugongo na kuongoza Ibada ya Shukrani.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch.Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amehitimisha ziara yake ya siku tatu ya kutembelea Jimbo la Pwani na Sharika zake kwa kuongoza Ibada ya Jumapili katika Usharika wa Maramba katika Jimbo la Pwani.

Rais wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF) Askofu Henrik Stubkjær ameungana na Watanzania katika kuadhimisha siku ya ugonjwa wa Hemophilia Duniani ambapo jamii imeaswa  kupima mara kwa mara ili kuweza kujua hali ya Afya zao na kuchukua hatua mapema.