Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, leo tarehe 30/06/2024 ameongoza Ibada ya Kustaaafu kwa heshima kwa Mch. Lewis Fredrick Shemkala  hii ikiwa ni kwa mujibu wa Katiba ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mchungaji Lewis Fredrick Shemkala, amefikia umri wa kustaafu baada ya kuitumikia Dayosisi hii kwa miaka 33 ya Uchungaji na miaka 2 ya Uinjilisti.

 

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch. Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amewashukuru Washarikwa wa Usharika wa Mlalo na wana KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kwa namna wanavyojitoa katika kumtumikia Mungu.

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ameupongeza uongozi wa Taasisi ya Elimu ya Kolowa Technical Training Institute (KOTETI), kwa kazi nzuri inayofanyika katika nyanja ya mafunzo kwa kuzingatia kasi na viwango katika utoaji wa Elimu katika taasisi hiyo inayomilikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.

Usharika  Mpya wa Bethania ni Usharika uliozaliwa kutoka katika Usharika Mama wa Kange. Usharika huu uliopo katika Jimbo la Pwani unaundwa na Mitaa miwili ambayo ni Mtaa wa SENTA pamoja na Mtaa wa PENUEL. Mtaa wa Senta upo katika maeneo ya Kange kasera karibu na Chuo cha Utumishi wa Umma na Mtaa wa Penuel upo katika maeneo ya Kasera. Mitaa yote hii miwili ilikua chini ya uangalizi wa Usharika mama wa Kange.