Msaidizi wa Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Michael Mlondakweli Kanju amesema kuwa kutokana na uwepo wa  mmomonyoko wa maadili katika jamii Kanisa limeona ni vema kuandaa mafunzo ya kuwajengea uwezo Wainjilisti wa Dayosisi ili wakawe chachu na kutatua changamoto hiyo katika jamii.

Mch Dkt. Albrecht Philips kutoka Kanisa la Westphalia (Evangelical Church of Westphalia) Ujerumani pamoja na msafara aliombatana nao, wamehitimisha ziara yao ya siku mbili ya kuitembelea KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs), ikiwa ni pamoja na baadhi ya vituo vinavyo milikiwa na KKKT-DKMs, kwa lengo la kuona vituo hivyo vinavyofanya kazi ili kuweka nguvu ya pamoja katika kuviboresha ili viendane na wakati.

HABARI PICHA:
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, akiwa ameongozana na ugeni kutoka Kanisa la Westphalia (Evangelical Church of Westphalia) Ujerumani, unaoongozwa na Mch Dkt. Albrecht Philips.
 
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amewataka Wachungaji waliobarikiwa pamoja na Watumishi wengine wa Kanisa kuendelea kukemea matendo maovu na mafundisho potofu ya neno la Mungu yaliyotanda katika jamii na ulimwengu kwa ujumla ili kuwezesha jamii kuendelea kuishi kwa amani na utulivu.