Uncategorised
- Details

- Details

MATUKIO KATIKA PICHA: Ibada ya uwekwaji wa Jiwe la Msingi la Kanisa katika Jimbo la Pwani,Usharika Mteule wa Ng’ambo ya Mto Pangani-Sange iliyoongozwa na Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu leo tarehe 17/11/2022.

Pamoja na uwekwaji wa jiwe la Msingi pia wameingizwa kazini Wazee wa Kanisa na viongozi wa kamati mbalimbali.
- Details

KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki mnamo tarehe 15/11/2022 ilipokea ugeni kutoka KKKT-Dayosisi ya Ulanga Kilombero kwa lengo la kujifunza na kudumisha undugu kati ya Dayosisi hizi mbili.
- Details

Leo tarehe 12/11/2022 imekuwa siku ya furaha na baraka tele kwa Washarika wa Usharika wa Malindi Mtaa wa Kana Mpya ambapo Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameongoza Ibada iliyokuwa na tendo la uwekwaji wa Jiwe la Msingi na ufunguzi wa Kanisa.

KATIKA HISTORIA:- Ibada katika Mtaa huu wa Kana Mpya, zilianza rasmi mwaka 2012 nyumbani kwa mzee Shabani Vuri kwa miaka mitatu mnamo mwaka 2015 Usharika ulipata eneo ambalo ndipo lilipojengwa Kanisa lililo funguliwa leo.
Page 66 of 124

