Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ametoa wito kwa wachungaji na watumishi wengine wa Kanisa kuwatambua watu wenye shida ya kusikia (viziwi) ili wasiachwe na ujumbe wa neno la Mungu unapohubiriwa.

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amemtambulisha Katibu Mkuu Mpya wa KKKT-DKMs Mwl. Julius Samweli Madiga kwa Washarika wa Jimbo la Pwani hususani wa Usharika wa Kange.

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu akiwa kwenye mazungumzo na mgeni wake, Katibu mtendaji wa idara ya mafunzo na uwezeshaji  kutoka UEM ,Mch Dkt. Andar Parlindungan mara baada ya kuwasili Makao Makuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki leo tarehe: 07/12/2022.

 UEM: United Evangelical Mission ni chama Cha kiinjili Cha kimisioni kilianzishwa mwaka 1996  na wamisionari kutoka Ujerumani wa Rhenish na Betheli ambao walifika Africa, na Asia kwa ajili ya kuanzisha shughuli za Dini. Katika Africa walifika katika nchi 7 ambazo ni Tanzania, DR Congo, Africa ya Kusini, Botswana, Cameroon, Namibia na Rwanda kukiwa na madhehebu 15. Katika Tanzania inawakilishwa na Makanisa 4 ya KKKT ambayo ni KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, KKKT Dayosisi ya Kaskazini Magharibi, KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani pamoja na KKKT Dayosisi ya Karagwe.

Aidha Chama hiki chenye miaka 26 sasa kinashughulika katika nguzo tano ambazo ni Uhusiano/ Undugu, Diakonia, Uinjilishaji, Utetezi pamoja na Maendeleo.

KATIKA PICHA: Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu (wa tatu kutoka kulia), Katibu mtendaji wa idara ya mafunzo na uwezeshaji Mch Dkt. Andar Parlindungan (wa pili kutoka kulia), Msaidizi wa Askofu KKKT-DKMs Mch. Michael Kanju (wa kwanza kutoka kulia), Katibu Mkuu KKKT-DKMs Mwl. Julius Samwel Madiga (wa pili kutoka kushoto), Naibu Katibu Mtendaji wa UEM  Kanda ya  Africa Mch Dkt. Ernest William Kadiva (wa tatu kutoka kushoto pamoja na Mkurugenzi wa fedha na Utawala KKKT-DKMs CPA. Peter Singano.

Leo tarehe 04/12/2022 Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameendelea na ziara yake nchini Sweden katika mji wa Uppsala (Cathedral) na ameshiriki kwenye Ibada ya kuingizwa kazini kwa Mkuu mpya wa  Kanisa la Sweden (The Church of Sweden), Askofu Dkt. Martin Modéus.

 Askofu Dkt. Mbilu ambaye pia amemuwakilisha Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Baba Askofu Dkt. Fredrick Onael Shoo kwenye Ibada hiyo.

Mkuu wa KKKT anakupongeza sana kwa kuchaguliwa na kuingizwa kazini kuwa Mkuu mpya wa Kanisa la Sweden.Tunakutakia baraka tele za Mungu wakati huu wa kusimikwa kwako kuwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Sweden.

“Mungu wetu akupe nguvu na hekima zote  katika wajibu huu mkuu ulioupokea leo. Ni maombi na matumaini yetu kwamba urafiki na ushirikiano wetu wa muda mrefu na mzuri utaendelea chini ya uongozi wako. Sisi wa KKKT tunakuahidi kukuombea na kukupa ushirikiano wa kutosha.

Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso” (Zaburi 46:1).

Ibada hiyo imehudhuriwa na Maaskofu kutoka mataifa mbalimbali duniani ikiwemo, Norway, Finland, Denmark, USA, Tanzania pamoja na Ethiopia. Pia Katibu Mkuu wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF), Katibu Mkuu wa Fungamano la Makanisa Duniani (WCC) pamoja na  Präses wa Kanisa la Westphalia (EKD) Annette Kurschuss  ni miongoni mwa watu walioshiriki katika Ibada hiyo.

 Askofu Martin Modéus alipata asilimia 59 ya kura katika uchaguzi  wa Askofu Mkuu uliofanyika tarehe 08/06/2022 hivyo amekuwa Askofu Mkuu mpya wa Kanisa la Sweden, akimrithi mtangulizi wake Askofu Antje Jackelen, ambaye alistaafu tarehe 30 Oktoba ya mwaka huu.

Askofu  Modéus anakuwa Askofu Mkuu wa 71 wa Kanisa hilo katika mlolongo usiokatika tangu Askofu Mkuu wa kwanza, Askofu Stephanus, mwaka 1164.