Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Mhe.Januari Lugangika ametoa wito kwa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kupitia Dayosisi zake 26 kuweka kipaumbele kwenye agenda ya kukifufua Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa (SEKOMU) kwani licha ya Chuo hicho kuwa na sifa ya kutoa taaluma bora na ya kipekee kimekuwa ni alama ya utume wa Kanisa kwa jamii.

Askofu Mteule wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch.Dkt.Msafiri Joseph Mbilu leo tarehe 11 Aprili, 2021 ameendelea kukutana na kufanya kikao na marafiki,wadau na wanadayosisi wanao ishi   katika Mkoa wa Arusha na maeneo ya jirani katika ukumbi wa mikutano wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Kati Usharika wa Engarenarok lengo likiwa ni  kuwapa taarifa juu ya hali ya Dayosisi ya Kaskazni Mashariki.