Uncategorised
- Details

Askofu Mteule wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, leo ameendelea kutambulishwa katika sharika mbalimbali za Dayosisi ambapo leo ameshiriki ibada ya Jumapili katika usharika wa Soni Jimbo la Kusini huku akiwataka waumini wa usharika huo kuanzisha miradi mbalimbali itakayowainua kiuchumi.

- Details

Askofu Mteule Mch. Dr. Msafiri Mbilu na viongozi wengine wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki pamoja na uongozi wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa SEKOMU wamemtembelea Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa .

- Details

Kikao cha tathmini ya kazi za Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMS) ambacho kimeanza kufanyika leo hii tarehe 6-9/01/2021 kimefunguliwa na Dean Mteule Mch Michael Kanju kwa niaba ya Askofu Mteule Mch Msafiri Joseph Mbilu ambaye katika utangulizi wa semina hii alisoma neno kuu la mwaka KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kutoka kitabu cha Zaburi: 32:8 “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea;Nitakushauri, Jicho langu likikutazama”.
Malengo ya kikao hiki ni kuweka vipaombele vya Dayosisi kwa mwaka 2021
Page 121 of 124


