Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, anasikitika kutangaza kifo cha Mchungaji Mstaafu Daniel Magogo, kilichotokea tarehe 16/05/2024, nyumbani kwake Kwesimu Lushoto Tanga.

Marehemu Mchungaji Mstaafu Daniel Magogo katikauhai wake alishawahi kuwa Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (Church President) kati ya mwaka 1965-1970.

Ibada ya mazishi  itafanyika katika Usharika wa  Kanisa Kuu Lushoto siku ya Jumatatu ya tarehe 20/05/2024 saa 4:00 Asubuhi.Na mara baada ya Ibada mwili wa Marehemu Mchungaji Mstaafu Daniel Magogo utapumzishwa katika makaburi ya familia yaliyopo Kwesimu Lushoto Tanga.

Tunamshukuru Mungu kwa mema mengi tuliyopokea kutoka kwa Mtumishi wake huyu.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana na lihimidiwe.