NENO KUU: JIANDAE KWA HUKUMU YA MWISHO

NENO LA MAHUBIRI: Mathayo 25:14-30

UTANGULIZI

Leo ikiwa ni jumapili ya pili (2) kabla ya kuingia katika kipindi cha MAJIRIO, majira ambayo wakristo wote ulimwenguni wanayaangalia mambo makubwa mawili 1. Kukumbuka ujio wa kwanza wa Bwana Yesu hapa ulimwenguni ambapo miaka zaidi ya 2000 iliyopita alizaliwa na kuleta ukombozi kwa kila mtu aliyemuamini na wanaoendelea kumuamini hata sasa. 2. Jambo la pili ambalo sisi wakristo tunaliangalia katika majira haya ni maandalizi yetu kwa ajili kumpokea Bwana Yesu katika ujio wake wa pili, ambapo analijia kanisa lake katika hukumu ya mwisho.

HABARI KWA UFUPI:Ibada ya Jumapili Sikukuu ya Watakatifu iliyoongozwa na neno kuu lisemalo sisi ni wenyeji wa Mbinguni, Ibada imefanyika leo tarehe 03/11/2024 katika Jimbo la Tambarare Usharika wa Muheza na kuongozwa na Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu.
 
Tarehe 02/11/2024 Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, alipatanafasi ya kuitembelea SACCOS ya Tumaini KKKT Handeni Savings and credit co-operative Society Ltd, iliyopo katika Jimbo la Magharibi Usharika wa Handeni kwa lengo na kuona namna SACCOS hiyo inavyoendeshwa.

Ikiwa leo tarehe 27/10/2024, katika  Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, ni Siku ya Kukumbuka Matengenezo ya Kanisa (Reformation) Askofu Dkt. Mbilu amesema kuwa Kanisa litaendelea kukemea mafundisho potofu yaliyotanda katika ulimwengu na kuendelea  kusimama katika msingi wa kuihubiri kweli ya Kristo.