Uncategorised
- Details
KATIKA PICHA KUTOKA JIMBO LA KASKAZINI USHARIKA WA KIRETI MTAA WA MPANDA: Ibada ya Jumapili ya leo tarehe 06/10/2024 iliyoambatana na Kubarikiwa kwa Vijana wa Kipaimara 133 na watu wazima 3 kubatizwa iliongozwa na Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu.

Vijana waliobariki katika kuonesha utayari wa kuchangia Deni la Dayosisi walichangia kiasi cha shilingi 665,000 na kuwaomba wazazi na walezi kuwaunga mkono na baada ya kuungwa mkoni kiasi cha Tsh. 2,066,400 kilipatikana.

Katika kuendelea kudumisha urafiki kati ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki na Dayosisi rafiki ya Lund Sweden Usharika wa Kireti wametembelewa na marafiki zao kutoka Usharika wa Örkelljunga Dayosisi ya Lund Sweden na wameshiriki katika Ibada ya Kipaimara iliyofanyika katika Usharika huo wa Kireti Mtaa wa Mpanda.
- Details
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameiomba Serikali kuongeza jitihada katika uchunguzi wanaoufanya ili kuwabaini mapema na kuwachukulia hatua za kisheria wahusika wote wa vitendo vya utekaji na mauwaji ya watu hapa nchini.
- Details
KATIKA PICHA. Ibada ya Uzinduzi wa Jimbo jipya la Diaspora Uingereza litakalo simamia, Uingereza, Ulaya na Marekani. Katika Ibada hii iliyofanyika Jumapili ya tarehe 22/09/2024, katika Usharika wa IMANI READING UINGEREZA, Mch.Tumaini Kallaghe, aliingizwa kazini kuliongoza Jimbo hilo.


- Details
Tarehe 21/09/2024 Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, alianza sa ziara yake ya kikazi nchini Uingereza na alipata nafasi ya kuongoza Ibada iliyokuwa na tendo la kuwabariki Vijana wa Kipaimara katika Usharika wa IMANI READING UINGEREZA. Katika Ibada hiyo jumla ya vijana watatu walibarikiwa na mmoja alibatizwa.

Page 19 of 125


