Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Dkt. Msafiri Joseph Mbilu leo tarehe 19/09/2021 ameongoza Ibada ya Jumapili katika Usharika wa Soni Mtaa wa Kwangwenda, Ibada hii ilikuwa na tukio la Uwekwaji wa jiwe la msingi la kanisa  pamoja na harambee ya ujenzi wa Kanisa la mtaa wa kwang’wenda.

Katika harambee hio Jumla ya  shilingi milioni kumi na moja hamsini na moja elfu na miatano hamsini (11,051,550)  ilipatikana kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa hilo lililowekewa jiwe la msingi.

Picha rasmi ya Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ,wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, nakala halisi iliyochapishwa Inapatika Makao Makuu ya KKKT-DKMs. Kwa mawasiliana wasiliana nasi kupitia  This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. au 0764105944/0655449481

Picha hii ndio itatumika katika Ofisi zote za Sharika za KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki

Leo tarehe 12/09/2021 imekuwa siku ya baraka kwa washarika wa Usharika wa Kisosora Jimbo la Pwani. Ambapo imefanyika Ibada iliyokuwa na matukio mbalimbali vijana wapatao 19 wamepata kipaimara na wawili kati yao walibatizwa.

Uongozi wa Shule ya Seminari ndogo ya Bangala iliyopo Halmashauri ya Bumbuli Vuga inawatangazia nafasi za kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka wa masomo  2022 kwa vijana waliomaliza darasa la saba mwaka huu 2021, mtihani wa kujiunga utafanyika tarehe 11/09/2021 na tarehe 25/09/2021. fomu za kujiunga zinapatikana katika vituo vifuatavyo.

Shuleni Bangala,Tumaini Bookshoop(Lushoto),Korogwe , Muheza, Handeni, Makorora, Kana.Pia tuna nafasi chache za wanaopenda kuhamia katika shule yetu kwa kidato cha tatu.