Matukioa katika picha Ibada ya Jumapili ya tarehe 17/09/2023, katika  Usharika wa Źory  nchini Poland, ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ambapo  kutoka Bara la Afrika ni  Mjumbe pekee  kwenye Kamati ya Ibada na Muziki kwenye mkutano Mkuu wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF) unaoendelea nchini Poland .Wajumbe wa Mkutano huo  wamepata nafasi ya kushiriki Ibada ya Jumapili  kwenye sharika mbalimbali. Ujumbe mkuu wa Mkutano huu ni kutoka kitabu cha Waefeso 4:4-6 "MWILI MMOJA, ROHO MMOJA, TUMAINI MOJA".