Ufunuo 14:13 “Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao”.

 Leo tarehe 30/05/2022 imefanyika Ibada ya mazishi ya Marehemu  Bibi,Hilgati A. Kika katika Usharika wa Makorora Jimbo la Pwani. Marehemu Bibi,Hilgati  Kika katika uhai wake alikuwa muimbaji wa kwaya Kuu KKKT-DKMs Usharika wa Makorora.

 

Marehemu Bibi,Hilgati ambaye pia ni mama mdogo wa Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, mwili wake umepumzishwa katika makaburi ya Bombo area Jijini Tanga.

Marehemu Bibi Hilgati alizaliwa tarehe 01/07/1948 katika Kijiji cha Kwang’wenda Wilayani Lushoto aliitwa mbinguni alfajiri ya tarehe 28/05/2022 katika Hospitali ya Mkoa wa Tanga- Bombo.

Uongozi wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki unaendelea kutoa pole kwa,familia ya marehemu,Kwaya Kuu Makorora,   ndugu, jamaa na marafiki popote pale walipo. BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe.

 

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameendelea kuwa kumbusha Washarika wa Usharika wa Kange na Dayosisi kwa ujumla kuendela kuchangia Deni la Dayosisi na kusema kuwa taarifa ya michango hiyo itaendelea kutolewa kama ilivyo fanyika awali.

amewakumbusha Washarika hao leo tarehe 29/05/2022  ni siku ya Bwana kabla ya Pentekoste, SIKU YA CCT Neno Kuu (Sikia Kuomba kwetu) Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameongoza Ibada ya Jumapili katika Jimbo la Pwani Usharika wa Kange na kuwasihi Washarika na Wanadayosisi kuona umuhimu wa kutoa sadaka ya CCT.

KATIKA PICHA Ibada ya ndoa kati ya Mtheologia Jonathan Denisi Hiza na Bi. Neema Simoni Mbilu. iliyofanyika leo tarehe 28/05/2022 katika Usharika wa Pongwe Jimbo la Pwani. Ndoa hiyo imefungwa na Msaidizi wa Askofu Mch. Michael Mlondakweli Kanju akishirikiana na Mkuu wa Jimbo la Pwani Mch. Thadeus Ketto.

Katibu Mkuu wa KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Godfrey Tahona Walalaze kwa niaba ya uongozi wa KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki anasikitika kutangaza kifo cha Mzee Paul Kaijuka kilichotokea nyumbani kwake Korogwe tarehe 23/05/2022.
 
Marehemu Mzee Paul Kaijuka katika uhai wake aliwahi kuitumikia KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Masharika kama Mhasibu Mkuu na Mkaguzi wa ndani wa mahesabu ya Dayosisi kwa vipindi tofauti.
 
Mazishi yatafanyika siku ya Ijumaa tarehe 27/05/2022 yakitanguliwa na Misa fupi nyumbani kwake na baadae saa sita mchana itafanyika Misa ya Mazishi katika PAROKIA YA MTAKATIFU. AUGUSTINO MANUNDU-KOROGWE.
 
Uongozi unatoa pole kwa familia ya Marehemu Mzee Paul Kaijuka, ndugu, jamaa na marafiki popote pale walipo. BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na lihimidiwe.